Tuesday, November 19, 2013

SIMBA S.C YAMNASA KOCHA MZUNGU

Zdravko Logarusic raia wa Croatia.

Baada ya kuwatimua makocha wake, Abdallah Kibadeni na msaidizi wake, Jamhuri Kiwhelo ‘Julio’, Simba sasa imemchukua kocha Zdravko Logarusic raia wa Croatia.
Tayari Simba imemaliza mazungumza na kocha huyo na anatarajia kutua nchini hivi karibuni kwa ajili ya kusaini mkataba na mara moja kuanza kazi.Kabla ya hapo, Logarusic alikuwa kocha wa Gor Mahia ya Kenya aliyoifundisha kwa misimu miwili akisha nafasi ya pili.Msimu huu ulikuwa wa mwisho kabla ya kubwaga manyanga na kumuachia mikoba Bobby Willismson , ambaye kulikuwa na uvumi kwamba angekuja kuitumikia Simba S.C.