Tuesday, April 2, 2013

CHELSEA YAIPIGA MAN UNITED CHA NGURUWE KOMBE LA FA

Timu ya soka ya Chelsea imeisambaratisha timu ngumu ya Man united katika kombe la chama cha soka cha Uingereza FA kwa bao moja kwa nunge katika dimba la Stamford Bridge, ukiwa ni mchezo wa marudiano baada ya mchezo wa kwanza uliopigwa katika dimba la Old Trafford kuisha kwa matokeo ya sare ya 2-2.


 
Demba BA akifunga goli pekee

Katika mchezo huo uliohudhuriwa na watazamaji wapatao 40,704 walishuhudia mtanange wa kukata na shoka. Wenyeji walionja tamu ya mtanange huo pale Mshambuliaji raia wa Senegal Demba BA alipofunga goli maridadi baada ya kutanguliziwa pande murua na Juan Mata katika dakika ya 48 ya mtanange huo. Goli hilo lilidumu mpaka mtanange unamalizika na hivyo Man United kuondoshwa katika michuano hiyo ya FA na kuiacha Chelsea kusonga mbele.

Wachezaji wa Chelsea wakimpongeza Demba BA baada ya kuitengeneza Man United

Danny Welbeck akijaribu kumtoka Oscar
 
Chelsea 1-0 Man United