Monday, February 4, 2013

RATIBA KAMILI NUSU FAINALI,FAINALI NA MSHINDI WA TATU KOMBE LA MATAIFA YA AFRIKA 2013

KOMBE LA MATAIFA YA AFRIKA | RATIBA


SAA CAT (TZ, GMT+3)

Jumatano 06 Februari 2013
1 Mali v    Nigeria Moses Mabhida Stadium 18:00
2 Burkina Faso v    Ghana Mbombela Stadium 21:30

Jumamosi 09 Februari 2013
2 Loser SF1 v    Loser SF2 Nelson Mandela Bay Stadium 21:00

Jumapili 10 Februari 2013
1 Winner SF1 v    Winner SF2 National Stadium 21:00

NIGERIA YAIFUNGASHIA VIRAGO IVORY COAST,BURKINA FASO YAIONDOA TOGO

Timu za soka za Taifa za Nigeria na Burkina Faso zimefanikiwa kutinga katika hatua ya nusu fainali ya kombe la mataifa ya Afrika.
Nigeria"Super Eagles" wametinga hatua ya nusu fainali baada ya kuitungua timu ngumu ya Ivory Coast"Simba wa Teranga" katika mchezo uliopigwa katika dimba la Royal Bafokeng na kuhudhuriwa na mashabiki wapatao 25,000. Magoli ya nigeria yalifungwa na Emenike dk 42 na la pili lilifungwa na Mba dk ya 77, Huku lile la kufutia machozi la Ivory Coast likitupiwa kambani na Tiote dk 49 ya mchezo.

Burkina Faso wametinga hatua ya nusu fainali kwa kuiondosha timu ngumu ya Togo iliyokuwa ikiongozwa na Adebayor kwa goli moja kwa ubuyu, Goli likitupiwa kambani na Pitroipa dk 104 ikiwa ni muda wa nyongeza baada ya timu hizo kutoshana nguvu katika dakika 90. Katika mtanange huo uliomalizika kwa Togo kuondolewa katika michuano hiyo mikubwa barani Afrika mashabiki wapatao 27,000 katika dimba la Mbombela walishuhudia Togo wakifungasha virago na kurejea nyumbani.

Pisha weweeeeeeee

Hapa kazi tuuu


Mba muuaji wa goli pekee la Burkina Faso


Kweli tumetoka!!!!!!!!!!!???????????



Kocha wa Nigeria Steven Kesh akishangilia kutinga nusu fainali

Huendi kokote weweeeeeeeeee

Adebayor akimwaga "udambwidambwi"

Burkina Faso wakishangilia baada ya kutinga nusu fainali

Ivory Coast 1-2 Nigeria
Burkina Faso 1-0 Togo

MAN CITY "YANASANA" NA LIVERPOOL

Mabingwa watetezi wa ligi kuu England Manchester City jana walishindwa kuendeleza mbio za kuifukuzia Man U kileleni pale walipolazimishwa sare ya mabao 2-2 na Liverpool katika dimba lao la nyumbani la Ettihad katika mpambano uliohudhuriwa na mashabiki wapatao 47,301.

Alikuwa ni Edwin Dzeko alieanza kuzifumania nyavu za Liverpool katika dakika ya 22 kabla ya Daniel Sturridge kuwanyamazisha mashabiki wa Liverpool katika dakika ya 28 ya mchezo. Mpaka mapumziko matokeo yalikuwa 1-1.

Katika kipindi cha pili alikuwa ni Mchezaji mkongwe Steven Gerrard alietupia mpira kambani na kuandika bao la 2 kwa Liverpool katika dakika ya 72 na kuamsha nderemo na vifijo katika dimba la Ettihad huku wenyeji wakiwa wanaona haya, Ilikuwa ni dakika ya 77 pale Aguero alipowapatia hafueni wenyeji kwa kutupia kambani bao la kusawazisha.
Mpaka mwisho wa mchezo matokeo yalikuwa Man C 2-2 Liverpool.

Sturridge akifumua shuti lililoelekea moja kwa moja kambani

Nimeuaaaaa...Sturridge akishangilia goli

Imoooooo...Steven Gerrard akiachia nduki kuandika bao la pili


Nimeuaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa!!!

Aguero akishangilia goli baada ya kumzidi maarifa Mlinda mlango wa Liverpool Reina
 
Man C 2-2 Liverpool