Wednesday, January 30, 2013

LULU SASA TUPO NAE MTAANI


Msanii wa filamu nchini, Elizabeth Michael ‘Lulu’ (kulia) akiwa na mama yake, Luklesia Kalugila nje ya Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam baada ya kuachiwa huru kwa dhamana jana.

SHABIKI AKOJOLEA NDINGA YA BALOTELLI


Shabiki anayesadikiwa kuwa Man United akikojolea ndinga ya Balotelli


Baada ya kuikojolea mwingine akashusha suruali na akapanda nyuma ya "Boneti"

Gari aina ya Bentley yenye thamani ya paundi za Uingereza 160,000 inayomilikiwa na mshambuliaji mtukutu wa Manchester City ambae kwasasa amesajiliwa na AC Milan Mario Bawuah Balotelli, ilikojolewa na mtu anayeasadikiwa kuwa ni shabiki wa Manchester United ilipokuwa imepaki katika mgahawa ujulikanao kama Indian Restaurant Zouk uliopo katikati ya jiji la Manchester siku ya Jumapili jioni.

Shabiki mwingine alionekana akiungana na mwenzake kulifanyia uhalifu gari la Balotelli kwa kushusha suruali yake na kupanda nyuma ya Boneti huku akipiga kelele.
Shuhuda wa tukio hilo Michael Armorgie aliliambia gazeti la The Sun kuwa "Nilikuwa ninapita ndipo nikawaona vijana wawili wakifanya vituko kwenye gari la Balotelli,Sikuamini..mmoja alikuwa analikojolea na mwingine amepanda juu anaimba nyimbo za Manchester United".

Hii ndio ndiga ya Balotelli iliyokojolewa

DROGBA AMFUATA SNEIJDER GALATASARAY BALOTELLI ATUA AC MILAN

Galatasaray imemsajili aliyekuwa mshambulizi wa Chelsea Didier Drogba kutoka kwa klabu ya Shanghai Shenhua inayoshiriki katika ligi kuu ya Premier nchini Uchina.

Galatasaray inayocheza ligi kuu nchini Uturuki, imethibitisha kuwa Drogba amesaini mkataba wa miezoi kumi na minane na klabu hiyo.

Mchezaji hiyo mwenye umri wa miaka 34, kwa sasa yuko nchini Afrika Kusini kuiongoza kikosi cha Ivory Coast katika mashindano ya kuwania kombe la mataifa ya Afrika.

Kwa mujibu wa ujumbe uliotumwa na kampuni ya uhusiano bora inayomuakilisha mchezaji huyo Sports PR Company na kuchapishwa kwa mtandano wa kijamii wa Twitter, Drogba alisema anajiandaa kurejea tena katika michuano ya kuwania kombe la klabu binga barani ulaya kwa mara nyingine.

Galatasaray imefuzu kwa raundi ya muondoana ya kuwania kombe hilo na imepangiwa kucheza na FC Schalke 04 kutoka uUjerumani.

''Hii ni fursa nzuri ya kuichezea timu kubwa na ni nafasi ambayo siwezi kupuuza'' Alisema Drogba.
Agenti wam mchezaji huyo amesema, Drogba atajiunga la klabu hiyo ya Galatasaray baada ya kukamilika kwa michuano ya kuwania kombe la mataifa ya Afrika.

Drogba ni mchezaji wa pili wa hadhi ya juu kusajiliwa na Galatasaray baada ya Wesley Sneijder aliyejiunga na klabu hiyo kutoka klabu ya Inter Milan.

Drogba alijiunga na Shanghai Shenhua mwezi juna mwaka uliopita na ameifunga jumla ya magoli manane baada ya kucheza mechi kumi na moja.

Awali Drogba alitaka kurejea Ulaya kwa mkopo na klabu yake ya zamani ilikuwa imeanzisha mazungumzo ya kumsajili.

Lakini shirikisho la mchezo wa soka duniani FIFA lilipinga uhamisho huo, likisema kuwa linakiuka sheria za kimataifa kuhusu uhamisho na usajili wa wachezaji.

Mchezaji mwingine wa zamani wa Cheslea Nicolas Anelka huenda pia anajiandaa kukihama klabu hiyo ya Shenhua, baada ya kufanyiwa uchunguzi wa kimatibabu katika klabu ya Juventus.



Drogba katika uzi wa Shenhua


Wesley Sneijder

BALOTELLI ATUA AC MILAN

Mkurugenzi wa klabu ya AC Millan, Umberto Gandini amethibitisha kuwa klabu hiyo imemsajili mshambuliaji wa Manchester City Mario Balotelli kwa mkataba wa miaka minne na nusu.

Balotelli, 22, anatarajiwa kufanyiwa uchunguzi wa kimatibabu mjini Milan siku ya Jumatano kabla ya kusaini wake na klabu hiyo.

Inakisiwa kuwa AC Milan imemsajili mchezaji huyo kwa kitita cha pauni milioni 20.

Awali Manchester City ilianzisha mazungumzo na vilabu vya AC Milan na Juventus kuhusu uwezekano wa kumsajili mshambuliaji wake Mario Balotelli, na ripoti zinasema kuwa, Balotelli atauzwa ikiwa vilabu hivyo vitaweza kulipa fedha wanazo taka.

Klabu hiyo imesema mchezji huyo mwenye umri wa miaka 22, anakisiwa kugharibu pauni milioni ishirini na moja mbali na fedha zingine za ziada.

Balotelli hana haraka ya kuuzwa na Manchester City imesema haina mipango ya kupunguza mshahara wake ili aondoke.

Kinyume na matarajio ya wengi Balotelli amesafiri na wachezaji wa Manchester City watakaocheza na QPR katika mechi ya ligi kuu ya premir leo usiku.

Milan ilianzisha mazungumzo na Man City, kuhusu mchezaji huyo kutoka Italia na kuna ripoti kuwa klabu ya Juventus vile vile imewasilisha ombi la kutka kumsajili Balotelli, ambaye alijiunga na Manchester City Agosti mwaka wa 2010 kwa kitita cha pauni milioni 24.

 Mario Baruah Balotelli


Swaga za kitaani

Mapema siku ya Jumatatu, naibu kocha mkuu wa Man City, David Platt, alisema kuwa Balotelli hatajiunga na AC Millan mwezi huu.

Siku ya Ijumaa wiki iliyopita, kocha wa Man City Roberto Mancini, alikariri hana nia ya kumuuza kuwa mchezaji huyo kutoka Italia.

Balotelli ambaye amefunga goli moja baada ya kucheza mechi kumi na nne msimu huu, amekumba na kashfa nyingi tangu aliposajiliwa.

Tukio la hivi karibuni, likiwa mzozo kati yake na Mancini katika uwanja wao wa mazoezi mwanzo wa mwezi huu.

Makamu wa rais wa AC Milan Adriano Galliani amesema ikiwa Manchester City itapunguza bei ya mchezaji huyo, basi huenda wakamsajili.