Monday, December 3, 2012

TANZANIA STARS YATINGA NUSU FAINALI YAIBANJUA RWANDA

Robo fainali ya kwanza ya michuano ya Tusker kati ya Tanzania Stars na Rwanda umemalizika jijini Kampala katika dimba la Lupogo,na timu ya Tanzania Stars ikitinga nusu fainali kwa kuichapa Amavubi mabao mawili kwa bila. Shujaa wa leo ni Mwinyi Kazimoto alietengeneza pande la maana kipindi cha kwanza katika dakika ya 33 na Amri Kiemba kumalizia kwa kumchambua kipa wa Rwanda na kutupia kambani bao la kwanza.
Dakika ya 54 ilikuwa ni Mwinyi Kazimoto"Iniesta" aliepiga shuti kali lililomshinda kipa wa Rwanda na bila kupepesa njumu, bila kupepesa bukta John Bocco "Adebayor" akauwahi mpira na kuutupia kambani na kufanya mabao kuwa ni 2-0.
Wakati Tanzania inatinga nusu fainali ndugu zao Zanzibar muda huu wapo uwanjani wakipepetana na Burundi katika robo fainali ya pili katika dimba hilohilo la Lupogo jijini Kampala,Uganda.
KILIMANJARO STARS 2-0 Rwanda
Shughuli imemalizika jijini Kampala, Stars imetinga nusu fainali baada ya kuichapa Amavubi mabao mawili kwa bila. Shujaa wa leo ni Mwinyi Kazimoto alietengeneza pande la maana kipindi cha kwanza katika dakika ya 33 na Amri Kiemba kumalizia kwa kumchambua kipa. Dakika ya 54 ilikuwa ni Mwinyi Kazimoto aliepiga shuti kali lililomshinda kipa wa Rwanda na John Bocco "Adebayor" akauwahi mpira na kuutupia wavuni. Hongera Stars!
Wachezaji wa Tanzania wakishangilia goli lililofungwa na John Bocco(14)

ROBO FAINALI TUSKER TANZANIA,ZANZIBAR KUPENYA?

ROBO FAINALI YA MICHUANO YA TUSKER CHALLENGE CUP 2012 INAYOENDELEA UGANDA

Desemba 3, 2012

Tanzania Vs Rwanda Saa 8:00 mchana Lugogo

Zanzibar Vs Burundi Saa 10:00 jioni Lugogo

Desemba 4, 2012

Kenya Vs Malawi Saa 10:00 jioni Namboole

Uganda Vs Ethiopia Saa 1:00 usiku Namboole