Tuesday, November 27, 2012

R.I.P HUSSEIN RAMADHAN MKIETE "SHARO MILIONEA"

Msanii wa vichekesho na muziki wa kizazi kipya Hussein Ramadhan Mkiete a.k.a Sharo Milionea amefariki katika ajali ya gari iliyotokea kijiji cha Lusanga,Muheza mkoani Tanga Siku ya jumatatu ya tarehe 26/11/2012 majira ya saa mbili usiku.
Habari zilizothibitishwa na kamanda wa polisi wa mkoa wa Tanga Constatine Massawe. kifo cha Sharo Milionea kimesababishwa na ajali aliyoipata wakati gari yake aina ya Toyota Harrier ilipopasuka tairi na kugonga mti eneo la Maguzoni.
Mwili wa marehemu Sharo umehifadhiwa katika hospitali Teule Tanga kwa kusubiria taratibu za mazishi zitakazofanywa na ndugu wa marehemu, Mungu ailaze roho ya marehemu Hussein Ramadhan Mkiete a.k.a SHARO MILIONEA Mahala pema peponi,AMIN!


Marehemu Hussein Ramadhan Mkiete "SHARO MILIONEA" enzi za uhai wake.


Sharo Milionea akifanya shopping mwezi huu kabla ya kupata ajali iliyoondoa uhai wake.



VIDEO ZA NYIMBO ZA SHARO MILIONEA