Monday, November 26, 2012

MAN CITY, CHELSEA HAKUNA MBABE

Timu za soka za Chelsea na Man City ziliumana katika mwendelezo wa mbio za kuwania ubingwa wa ligi kuu ya Uingereza katika uwanja wa Stamford Bridge.
Katika mpambano huo wa wababe hao kutoka suluhu na ikiwa mechi ya kwanza kwa kocha mpya wa Chelsea Rafael Benitez akichukua nafasi ya kocha kipenzi cha mashabiki wa Chelsea Roberto De Matteo.
Mashabiki wa Chelsea hawakufurahishwa na kitendo cha De Matteo kutimuliwa na wameonesha kwa kiasi kikubwa hawamkubali kabisa Rafael Benitez ambaye ameshindwa kuipa matumaini mema Liverpool alipokuwa kocha mkuu na sasa yupo Chelsea itakuwaje? ngoja tusubirie lakini mashabiki na mimi mwenyewe hatumkubali Benitez kama tunavyomkubali De Matteo.




Mashabiki wa Chelsea na ujumbe wa kumdhihaki Benitez na kumtukuza De Matteo


Benitez akiwa kibaruani lakini mashabiki hawamkubali hata kidogo

Roberto Mancini kocha wa Man City akitoa maelekezo katika mpambano huo


Huu Haaa!! Kazi Vicent Company na Torres


Tulia wewe bwana mdogo tuu!!! Torres akiwa chini ya ulinzi mkali


Ukijipendekeza nakupasua!!! Ramires akimtuliza Aguero


Aaaah mi nimeshachoka msiniseme sana bhanaa wanakaba kama nini!!

MPIGIE KURA MCHEZAJI UNAYETAKA ACHUKUE TUZO YA MCHEZAJI BORA AFRIKA 2012 YA BBC

Majina ya wachezaji watano wanaowania tuzo la BBC la mchezaji bora zaidi barani Afrika mwaka 2012 yamewekwa hadharani.

Bofya Yahya Toure.
Mcheza kiungo kutoka Ivory Coast, anayeichezea Manchester City ya Uingereza. Toure aliiongoza Manchestert City kushinda kombe la ligi kuu ya Premier ya England kwa mara ya kwanza kwa zaidi ya miaka 44 iliyopita.


Bofya Demba Ba
kwa sasa ni mmoja wa wachezaji nyota wa klabu ya Newcastle na kufikia sasa tayari amefunga jumla ya magoli 6 katika ligi kuu ya premier la England na anatarajiwa kujumuishwa kwenye kikosi cha Senegal kitakachocheza katika fainali ya kombe la mataifa bingwa barani Afrika.


Bofya Didier Drogba
Ni noadha wa timu ya taifa ya Ivory Coast, amewahi kuongoza Chelsea kushinda kombe la ligi kuu ya Premier ya England pamoja na kombe la klabu bingwa barani ulaya.


Bofya Christopher Katongo
Ni mchezaji wa timu ya taifa ya Zambia maarufu kama Chipolopolo na aliiongoza timu hiyo kushinda fainali ya kombe la mataifa bingwa barani Afrika


Bofya Younes Belhanda
Ni mchezaji mwenye umri wa miaka 22, na mmoja wa wachezaji waliotia fora na kuisaidia klabu ya Montepellier, kushinda kombe la ligi kuu kwa mara ya kwanza kwa zaidi ya karne moja tangu klabu hiyo ilipobuniwa.

PIGA KURA HAPA
Bofya Ukitaka kupiga kura unaweza kufungua anwami hii ya mtandao na kumbuka maagiza yametolewa kwa lugha ya Kiingereza.