Wednesday, September 19, 2012

NGORONGORO CRATER "AFRICA'S GARDEN OF EDEN"

QUICK FACTS ABOUT NGORONGORO CRATER
  • Largest unbroken caldera in the world
  • Also referred to as "Africa's Garden of Eden"
  • Crater is 12 miles (19 km) across and covers 102 square miles (264 sq km)
  • Rises over 2,000 feet above the caldera floor
  • Home to over 30,000 animals including the rare black rhino


  • Ngorongoro Crater is the world's largest unbroken caldera. Often referred to as "Africa's Garden of Eden," the crater is home to over 30,000 animals including elephants, lions, cheetahs, wildebeests, buffaloes, and the rare black rhinos. View Wildlife of Ngorongoro Crater to learn more about the wildlife and View Birds of Ngorongoro Crater to discover some of the many species that are found in the area.
    Ngorongoro Crater was created from a volcano that exploded creating the caldera wilderness haven. The crater is 12 miles (19 km) across and consumes 102 square miles (264 sq km) of wilderness. The rim of the crater rises just over 2,000 feet (610 m) above the caldera floor reaching an elevation of 7,500 feet (2,286 m).






    OMMY DIMPLES- Baadae


    ARSENAL YAIADHIBU MONTPELLIER

    Arsenal imeanza vyema michuano ya ligi ya mabingwa hatua ya makundi baada ya kuichabanga Montpellier kwa magoli 2-1 nyumbani kwao katika dimba la La Mosson.

    Wenyeji ndio walikuwa wa kwanza kuzifumania nyavu za wageni kwa bao maridadi la mkwaju wa penati iliyopigwa na Belhanda katika dakika ya 8 ya mchezo.
    Watoto wa London,Arsenal "The Gunners" waliibuka kama mbogo aliejeruhiwa na kusawazisha goli katika dakika ya 15 likitupiwa kambani na Lucas Podolski.

    Mtanange uliendelea huku kila timu ikisaka bao la ushindi na kuthibitisha hilo karata zilichezeka vizuri upande wa Arsenal na katika dakika ya 17 Gervinho aliwainua vitini mashabiki wa Arsenal kwa kutupia kambani goli la pili.

    Mpaka mapumziko ngoma ilinoga kwa Arsenal kuwa mbele kwa kamba 2 kwa 1 ya Montpellier.Kipindi cha pili hakikuwa na mabadiliko ya matokeo ya mchezo huo uliohudhuriwa na mashabiki wapatao 30,000 katika dimba hilo la Montpellier, na mpaka kipyenga cha mwamuzi kinaenda hewani matokeo yalikuwa Montpellier 1-2 Arsenal.

    Podolski akitupia kambani goli la kusawazisha



    Podolski akishangilia goli la kwanza

    Hapa huendi kokote we mirasta!!!

    Gibbs akijaribu kupiga majaro langoni mwa Montpellier


    Gervinho akitupia kambani goli la pili

    Gervinho - Montpellier Herault SC v Arsenal FC - UEFA Champions League
    Gervinho akishangilia goli

    Montpellier 1-2 Arsenal

    REAL MADRID YAICHAPA MAN CITY KWA TAABU

    Vicent Company akijaribu kumzuia Christian Ronaldo asilete maafa
     
    Kamba ya  Cristiano Ronaldo katika dakika ya mwisho ya mchezo iliiwezesha klabu ya Real Madrid kuibangua Manchester City magoli 3-2 walipowakaribisha katika uwanja wao wa Bernabeu nchini Uhispania, mechi ya klabu bingwa barani Ulaya.

    Kipa Joe Hart alikuwa mwiba kwa Real Madrid na aliiwezesha Man City kuendelea vyema bila kufungana mabao katika mechi ya Jumanne usiku, hadi Edin Dzeko alipowashangaza wenyeji kwa kupata bao katika kipindi cha pili.

    Marcelo alisawazisha, kupitia mpira ambao ulimgusa mchezaji wa City kabla ya kubadilisha mwendo, lakini City wakafanikiwa kuendelea tena kuongoza baada ya mkwaju wa free-kick kutoka kwa Aleksandar Kolarov, wakati mpira moja kwa moja ulielekea hadi wavuni.
    Kisha Karim Benzema aliweza kusawazisha, kabla ya Ronaldo kuandikisha bao la tatu na la ushindi katika mechi hiyo, na matokeo yakawa 3-2.

    Kati ya mechi nyingine za klabu bingwa barani Ulaya ilikuwa ni pamoja na mchezo wa Arsenal, ambayo ilianza kampeni yake ya 15 ya mashindano hayo kwa kuwashinda wageni katika michuano hiyo, Montpellier ya Ufaransa.

    Timu ya Arsene Wenger ililemewa ugenini baada ya dakika tisa, wakati nahodha Thomas Vermaelen aliposababisha penalti,ambayo ilifungwa na Belhanda, lakini kutokana na magoli mawili ya Arsenal kupatikana kwa haraka katika kipindi cha kwanza, kutoka kwa Lukas Podolski na Gervinho, hali ya mchezo ilibadilika, na Arsenal ikapata ushindi wa magoli 2-1.

    Ushindi huo unamaanisha Arsenal na Schalke ya Ujerumani ndio vilabu ambavyo vinaongoza katika kundi B.

    Shughuli pevu...Khedira na Kolarov

    Yaya Toure akipasua mawimbi huku Essien akimfuatilia kwa karibu zaidi


    Tevez chini ya ulinzi mkali


    Edwin Dzeko akishangilia bao la pili



    Mourinho na Ronaldo wakishangilia goli la tatu na la ushindi lililofungwa na Christiano Ronaldo kwa staili ya kufanana.


    Ndio mpira kaka "FAIR PLAY" Mancini na Mourinho wakisalimiana kabla ya mpambano kuanza

    REAL MADRID 3-2 MAN CITY