Friday, September 14, 2012

SHILOLE AFUNGUKA ALIVYOBAKWA NA KUPACHIKWA MIMBA


Zuwena Mohamed "Shilole"

Msanii wa Filamu za kibongo "Bongo Movies" na muimbaji wa Nyimbo za kibongo "Bongo Flavour" Mwanadada Shilole amefunguka jinsi jamaa lenye uchu lilivyombaka na kumtoa bikra na ujauzito juu.

Shilole akielezea historia ya maisha yake katika kipindi cha Leo tena kinachendeshwa na Dina Marios kupitia kituo cha Radio cha Clouds Fm cha jijini Dar es salaam, amefunguka kwa kuelezea majaribu aliyokutana nayo kuanzia utoto wake kuelekea ukubwani.
Pamoja na mapito yote ikiwamo kunyanyaswa na kuteswa na wifi na shemeji zake aliowahi kuishi nao kikubwa zaidi katika mapito hayo ni jinsi alivyobakwa na hatimae kutolewa usichana wake"Bikra" na kupata ujauzito.

Majaribu hayo yalimpata mwanadada Shilole alipokwenda kuchota maji majira ya usiku kipindi anaishi na ndugu zake huko Igunga mkoani Tabora. Akielezea mkasa huo Shilole anasema kwa uchungu na hisia kali kuwa siku ya tukio alikuwa amekwenda kisimani kuchota maji." Nilikuwa nimeenda kuchota maji usiku ndipo ghafla akatokea jamaa na kunikamata kwa nguvu, nikajaribu kupiga kelele hazikusikika na akawa ameshatimiza haja yake" Alielezea.

"Nilipata wakati mgumu kurudi nyumbani na kuelezea kilichotokea" aliendelea. Akielezea mkasa huo pamoja na kubakwa alipofika nyumbani na kuelezea tukio hilo alipokea kipondo kitakatifu na akidaiwa kuwa ndio ulikuwa mchezo wake, alijaribu kukataa lakini haikusaidia kitu aliendelea kupata kipondo mpaka mtoa kipondo aliporidhika.

Mwisho wa siku akiwa na ujauzito na kutafakari sana katika maisha magumu, huku akitaka kuitoa lakini mwisho wa siku aliendelea kufanya biashara mitaani na mwisho wa siku akajifungua salama salmini, mtoto huyo wa kwanza anaitwa Rahma.

Mtoto wa kwanza wa Shilole,Rahma

Shilole na Masanja mkandamizaji


Shilole jukwaani


Shilole akiwajibika jukwaani na wacheza shoo wake


Shilole na JB


Shilole katika Pozi matata

AUNT EZEKIEL "KUFULI" NJE NJE HAPANA CHEZEA YEYE


Aunt Ezekiel katika tamasha la Serengeti Fiesta 2012



Aunt Ezekiel na Steve Nyerere katika tamasha la Serengeti Fiesta 2012


Kama mgongo ninao..mnasemajeeeee?


Mauno timeee..Aunt akimwaga mauno mbele ya Steve Nyerere katika tamasha la Serengeti Fiesta 2012