Monday, September 10, 2012

SIMU YA MKONONI NI HATARI KWA MAISHA YAKO,TAFADHALI ITUMIE KISTAARABU

Fun & Info @ Keralites.net
Hawa wanapata kahawa jioni lakini maongezi hakuna kila mtu bizee na kisimu chake


Fun & Info @ Keralites.net
Wapo Dinner lakini kila mtu kwenye simu jamani kunaniii simuni?

Fun & Info @ Keralites.net
Wamekaa wanamsubiri mgeni hotelini lakini hakuna stori ni simu tuu..khaaa!!!??

Fun & Info @ Keralites.net
Wamekutana chakula cha usiku"Dinner" mhhh biiizee na simu no stori hapa

Fun & Info @ Keralites.net
Marafiki wapo Ufukweni "Beach" lakini hakuna stori, hakuna kucheza wala kuogelea ni simu tuuu..mweeee!!!

Fun & Info @ Keralites.net
Haya sasa mtu yupo uwanjani hafuatilii tena mechi ni simu tuuu bhaaaah!!

Fun & Info @ Keralites.net
Hawa ni wapenzi wametoana "OUT" badala ya kubadilishana mawazo kudumisha penzi lao
kazi ni moja simuuu heeee!!

Fun & Info @ Keralites.net
Misere na ndinga kitaani No stori ni simu tu kuchata kwa kwenda mbele kaazi kwelikweli

Fun & Info @ Keralites.net
Shughuli sasa hii hapa, Wanapoendesha magari ni simu tuuu vimeseji mwisho wa siku wanasababisha ajali...jamani mhhh ukistaajab ya Khalid Utayaona ya Firauni.

Fun & Info @ Keralites.net
Achana na waendesha magari shughuli pia imo kwa watembeaji kwa miguu na waendesha baiskeli, umeonaaa ni simu tuuu kudadadadekii utakoma mwenyewe ni kikumbo tu ukizubaazubaa!!

OBAMA ABEBWA JUU JUU NA MUUZA PIZZA


Rais Obama akiwa amenyanyuliwa juu na Scott Van Duzer

Mmiliki wa Mgahawa maarufu jijini Florida, Marekani Scott Van Duzer alitoa kali ya mwaka alipotembelewa na Rais Obama katika mgahawa wake na kumnyanyua juu kama ishara ya furaha aliyikuwa nayo kwa ujio wa Obama pale mgahawani.

Rais Obama akitumia usafiri wa basi katika ziara ya siku mbili jijini Florida ikiwa ni sehemu za kampeni za uchaguzi utakaofanyika mwezi Novemba, alitembelea Mgahawa maarufu jijini Florida unaotambulika vilivyo kwa kuuza Pizza baaab kubwa unaojulikana kama Big Apple Pizza & Pasta Restaurant unaomilikiwa na Scott Van Duzer.

"Scott, what's going on, man," alisikika rais Obama akisalimiana na Van Duzer mara tu ya kuingia mgahawani. "Let me tell you, you are like the biggest pizza shop owner I've ever seen."  Obama aliendelea kumwaagia misifa Van Duzer ambae alimpigia kura rais Obama mwaka 2008 na ameahidi kumpigia tena kura mwezi Novemba.


Woooowww jamani rahaaa sio rahaaaa...Van Duzer akimkumbatia President Obama na kumnyanyua juu juu katika mgahawa anaoumiliki wa Big Apple Pizza & Pasta Restaurant jijini Florida,Marekani.

RICH MAVOKO- Marry ME


MAKAMO WA RAIS AHUKUMIWA KIFO

TariQ Al Hashemi
 
Mahakama nchini Iraq imepitisha hukumu ya kifo kwa makamu wa rais, Tariq al-Hashemi, baada ya kumkuta na hatia kwa kuongoza makundi ya kuuwa watu, yaliyowalenga Washia na askari wa usalama.
Makamo wa rais, wa madhehebu ya Sunni, hakuweko mahakamani wakati wa hukumu hiyo kwani alishaikimbia Iraq awali mwaka huu, akiwa sasa anaishi Uturuki.

Kesi hiyo imezusha msukosuko wa kisiasa katika serikali ya Iraq, iliyogawa madaraka kati ya Wa-Sunni, wa-Shia na WaKurd.

Bwana al-Hashemi amemshutumu Waziri Mkuu Nuri al-Maliki ambaye ni M-Shia, kuwa anawasaka wapinzani wake wa kisiasa wa madhehebu ya Sunni, lakini serikali inasisitiza kuwa kesi hiyo inafuata misingi ya sheria tu.


Hukumu hii ya mahakama imekuja huku watu wasiopungua 45 wakiwa wameuawa katika mfululizo wa mashambulizi 24 nchini Iraq. Siku ya Jumapili mashambulizi kadhaa yalishuhudiwa katika maeneo ya Tuz Khurmatu, Baquba, Basra na Samarra.

Wanajeshi 11 waliuawa kaskazini mwa Baghdad, huku katika mji wa Amara watu 14 wakiuawa na wengine 60 kujeruhiwa katika mashambulio mawili ya mabomu ya kutegwa katika gari.

Maafisa polisi saba pia waliuawa kwa bomu katika mji wa kaskazini wa Kirkuk, wakati wanajeshi kumi nao wakiuawa katika kambi ya jeshi ya Dujail kaskazini mwa Baghdad. Na katika eneo la Nasiriya kusini kulitokea mlipuko wa bomu nje ya ubalozi wa Ufaransa ulioua mtu mmoja huku serikali ya Ufaransa ikilaani shambulio hilo.

Hashimu alikuwa ni mwanasiasa wa juu sana aliyeheshimika kutoka dhehemu la Sunni katika serikali yenye Wa-Shia wengi hadi alipofunguliwa mashitaka mwezi December mwaka 2011 wakati alipotoroka nchini humo.

Wanasiasa wengine wa Ki-Sunni walimkataa waziri mkuu wa Ki-Shia Nouri al-Maliki aliyetoa amri ya kukamatwa kwa Bwana Hashemi, wakimuita kama dikteta na kumshutumu kwa kuendeleza chokochoko zinazoweza kuiingiza nchi hiyo katika vita vya kikabila kwa mara nyingine.

Waandishi wa habari wanasema muungano wa serikali kati ya Wa-Sunni, Wa-Shia na wale wa makabila mengine inaonkena kuwa hatarini tokea wakati huo.

Wapiganaji wa Ki-Sunni wanaohusishwa na kundi la kigaidi la al-Qaeda wamekuwa wakishutumiwa kwa vurugu za hivi karibuni nchini Iraq.