Monday, September 3, 2012

ROBIN VAN PERSIE APIGA "HAT TRICK"

Robin Van Persie Robin Van Persie of Manchester United celebrates the winning goal during the Barclays Premier League match between Southampton and Manchestrer United at St Mary's Stadium on September 2, 2012 in Southampton, England.
Van Persie
 
Robin van Persie amegeuka kuwa kipenzi cha mashabiki wa klabu yake mpya kwa kuiokoa Man.United alipofunga matatu mwenyewe kumuondolea maradhi ya moyo Sir Alex Ferguson kunako mechi yake ya 1,000th akiiongoza Manchester United kama meneja.

Mdachi huyo alitanguliza la kichwa kutokana na kona iliyochongwa na Nani katika mda wa ziada kuokoa jahazi.

Southampton ilipata bao la kuongoza kupitia Rickie Lambert kabla ya Morgan Schneiderlin kupata la pili pia la kichwa katikati ya magoli ya Van Persie ya kusawazisha.

Uhodari wa Van Persie uliwekwa kwenya mizani alipokosa mkwaju wa peneti mnamo dakika 88 wakati United ikidorora 2-1.

Kwa menejawa Southampton Nigel Adkins dakika za majeruhi zilikua kama mwaka wenye machungu kutokana na jinsi vijana wake walivyoweza kuidhibiti United na mabao ya haraka haraka mawili bila shaka yalimuumiza.

Kwa mashabiki wa United, matokeo haya ni sehemu ya malipo ya kitita cha milioni 24 za pauni za Uingereza zilizomleta United kutoka Arsenal.
Robin Van Persie Robin Van Persie of Manchester United scores the winning goal during the Barclays Premier League match between Southampton and Manchestrer United at St Mary's Stadium on September 2, 2012 in Southampton, England.
Van Persie akitupia goli la kwanza
Robin Van Persie Robin Van Persie of Manchester United scores his second goal during the Barclays Premier League match between Southampton and Manchestrer United at St Mary's Stadium on September 2, 2012 in Southampton, England.
Van Persie akitupia goli la pili
Robin Van Persie Robin Van Persie of Manchester United celebrates the winning goal during the Barclays Premier League match between Southampton and Manchestrer United at St Mary's Stadium on September 2, 2012 in Southampton, England.
Van Persie akishangilia bao
Robin Van Persie Robin Van Persie of Manchester United scores the winning goal during the Barclays Premier League match between Southampton and Manchestrer United at St Mary's Stadium on September 2, 2012 in Southampton, England.
Mpira uliopigwa na Van Persie ukitinga wavuni kuandika goli la tatu "Hat Trick" na la mwisho la Man United
Southampton vs Man United

ARSENAL YAANZA LIGI YAIDUNGUA LIVERPOOL 2 KAVU


Kocha wa Arsenal Arsene Wenger akizungumza na waandishi wa habari baada ya mechi.

Arsenal imepata ushindi wake wa kwanza katika ligi ya Premier ya nchini Uingereza msimu huu baada ya kuidungua Liverpool 2-0 nyumbani kwao.
Hii ndio mara ya kwanza kabisa kwa Liverpool kuanza msimu kwa kichapo cha mabao 2-0 katika uwanja wao katika kipindi cha miaka 50,Magoli yote mawili ya Arsenal yalitupia kambani na wachezaji wapya Santi Cazorla na Lukas Podolski .

Mshambuliaji wa Ujerumani Podolski ndiye alikuwa wa kwanza kuipatia Arsenal bao katika dakika ya 31. Na katika dakika ya 68 Cazorla alipeleka kilio na kubadili ubao wa matangazo kuwa 2-0.
pod_2326586c.jpg
Podolski akitupia goli la kwanza

Podolsi akishangilia goli

Magoli hayo pia ndio yalikuwa ya kwanza kwa Arsenal tangu msimu huu uanze kwani katika mechi zao mbili za awali walitoka sare ya 0-0 na wapinzani wao.

Kufuatia ushindi huo Kocha wa Arsenal alisema kuwa uimara wa vijana wake unaongezeka katika kila mechi na kuwa amefurahishwa na matokeo ya timu yake.

Baada ya kucheza mechi tatu, Liverpool ambayo iko nchini ya mkufunzi mpya Brendan Rodgers ina pointi moja peke yake.

Hii inaweza kufananishwa na matokeo mabaya ya timu hiyo katika msimu wa mwaka 1962-63 chini ya Bill Shankly.

Katika mechi hii washambulizi Luis Suarez na Fabio Borini hawakuwa na kubwa uwanjani.

Nae mchezaji mpya wa kiungo Nuri Sahin wa Liverpool pia hakuonyesha makeke yake uwanjani.

Santiago Carzola akishangilia baada ya kutupia goli la pili


Golikipa wa Arsenal Manone akishangilia ushindi


Patashika Steven Gerrard na Abou Diaby

Liverpool 0-2 Arsenal