Tuesday, July 10, 2012

Wimbo wa leo BOB JUNIOR-Nichum

MPAMBANO WA SOKA WABUNGE WA SIMBA NA YANGA KATIKA PICHA


Timu za wabunge wa Simba na Yanga wakiimba wimbo wa Taifa kabla ya mpambano

Waamuzi wa mpambano huo wakipiga picha ya pamoja na manahodha wa timu zote mbili

Wabunge wa Simba katika Dua kabla ya mtanange kuanza


Wabunge wa Yanga nao wakipiga dua kabla ya mtanange kurindima

Mashabiki wakiwahi mpambano

Mtanange umeanza


Mwamuzi wa mtanange huo Athuman Kazi akifuatilia kwa karibu kuhakikisha haki inatendeka


Mh Zitto Kabwe wa Simba akitoa pasi murua kama Iniesta vile!


Mbunge wa Simba akitiririka na kabumbu















Katibu uenezi wa CCM Nape Nnauye akifuatilia mpambano wa Wabunge wa Simba na wale wa Yanga katika dimba kuu la Taifa jijini Dar es salaam


Benchi la ufundi la Wabunge wa Simba wakifuatilia mpambano


Benchi la ufundi la Wabunge wa Yanga wakiongozwa na kocha mkuu mpya wa Yanga


Mbunge wa Yanga akiwa hoi bin taaban


Mbunge wa Yanga akijaribu kuihadaa ngome ya wabunge wa Simba


Hali tete mlinda mlango wa wabunge wa Yanga baada ya kichapo kwa njia ya matuta 3-2


Wera weraaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa!!! wabunge wa Simba hatimae waliwachapa wa Yanga katika matuta baada ya dakika 90 kumalizika kwa sare ya 0-0




Nani kama Simbaaaa woyooooo woyooooooooo


Hakunagaa zaidi ya Simba hakunagaa, hakunaaa hakunaaaa hakunaaaaaaaaaa!!!


Weraaaaa tupishe tupiteeee, tupisheeeee tupishe tupiteeeeeeee..Wabunge wa Simba wakiongozwa na Mh Zitto Kabwe na William Ngeleja kuserebuka baada ya kuwaangushia kisago wenzao wa Yanga kwa mikwaju ya penati 3-2
Mpambano Wabunge SIMBA Vs YANGA

Katika mtanange huo baada ya dakika 90 na kipyenga cha mwamuzi Athumani kazi kupulizwa matokeo yalikuwa ni 0-0. Mpambano huo wa kufurahisha na kusisimua uliopigwa katika dimba kuu la Taifa jijini Dar es salaam ikiwa ni katika mchezo wa hisani kukusanya pesa kuchangia ujenzi wa mabweni kwa shule za sekondari nchini!

shukrani za pekee kwa waandaaji wa tamasha hilo ambalo pia liliwakutanisha wasanii wa Bongo flava na Bongo Movie hali kadhalika mpambano wa Masumbwi kati ya wasanii maarufu nchini na wenye kutengeneza vichwa vya habari katika redio na magazeti mbalimbali hapa nchini, ni Wema Sepetu na Jaquiline Wolper ambapo katika mpambano mpambano huo uliodumu kwa raundi mbili matokeo yalikuwa ni droo hakukuwa na mshindi.

KEITA AONDOKA BARCELONA NA "NDOO"14 HUKU TITO AKIMRITHI PEP GUARDIOLA


Seydou Keita

kiungo wa Mali Seydou Keita amekihama klabu ya Barcelona baada ya kukipiga kwa miaka minne.
Katika muda huo wa miaka minne, Keita aliisaidia Barcelona kuzoa jumla ya vikombe 14.
Wakati wakithibitisha kuondoka kwa mwamba huyo, Barca walimshukuru Seydou Keita kwa juhudi zake za kuiletea klabu hiyo ya Uhispania mafanikio na vile vile wakamtakia kila lakheri anakokwenda.

Keita na Sanchez wakiwa wamebeba kombe wakikipiga Barcelona

Kwa wakati huu kuna fununu kwamba mchezaji huyo wa Mali huenda anahamia klabu moja ya Uchina, Dalian Aerbin
Ikiwa hatiamae ataishia China basi Keita hatakuwa mchezaji wa kwanza kutoka bara la Afrika kufanya hivyo.
Majuzi nahodha wa timu ya Ivory Coast Didier Drogba aliwafuata Frederic Kanoute na Yakubu Aiyegbeni wa Nigeria kujiunga na timu za ligi kuu ya China.
Keita, mwenye umri wa 32, alijiunga na Barcelona mwaka 2008 kutoka Sevilla akiwa ni mchezaji wa kwanza kabisa ambaye Pep Guardiola alimsajili mara tu alipokwaa uongozi wa Barca.
Kabla ya hapo mchezaji huyo alikuwa Olympic Marseille, Lorient na Lens zote za Ufaransa na ndio baadaye akahima Seville ya Uhispania.
Keita amehama baada ya Guardiola kuondoka kama Meneja wa Barcelona na mahali pake kuchukuliwa na aliyekuwa naibu wake Tito Vilanova

Tito Vilanova kocha alierithi mikoba ya Pep Guardiola


Tito Vilanova akiwa na Pep Guardiola