Tuesday, June 5, 2012

FAHAMU KWA UNDANI NCHI, MIJI, VIWANJA MICHUANO YA EURO 2012


POLAND
City
Stadium
Capacity
ChorzówSilesia Stadium50,000
WarsawNational Stadium55,000
PoznańMunicipal Stadium46,000
WrocławStadium in Maślice44,000
GdańskBaltic Arena44,000
KrakówWisła Stadium35,000

Ukraine

City
Stadium
Capacity
KyivNSK Olimpiyskyi73,000
DonetskShakhtar Stadium50,000
KharkivMetalist Stadium42,000
LvivUkraina Stadium32,000
OdesaChornomorets Stadium34,362
DnipropetrovskDnipro Stadium34,000

HAZARD ATUA CHELSEA


Eden Hazard

Klabu ya soka ya England ya Chelsea imetangaza katika tovuti yake kwamba hatimaye imekubaliana na klabu ya Lille ya Ufaransa kwamba mchezaji wa kimataifa ya Ubelgiji, Eden Hazard, atajiunga na klabu hiyo ya Stamford Bridge msimu ujao. Mchezaji huyo, mwenye umri wa miaka 21, tayari afya yake imekaguliwa na klabu ya Chelsea, na imeonekana hana tatizo lolote.

Walipochukua ubingwa wa ligi ya klabu bingwa, nilijiuliza, "Kwa nini sio Chelsea?", alisema Hazard.

"Kulikuwa na mvutano kati ya Chelsea na Manchester united, lakini binafsi naona Chelsea ndio mradi bora zaidi. Ni klabu cha ajabu."


Eden Hazard

Inaarifiwa kwamba Chelsea wameamua kutoa pauni milioni 32 kumpata kijana huyo, na ambaye akizungumza na kituo cha redio cha nchini Ufaransa, RMC, aliongezea: "Chelsea ni timu changa, na nitakuwa na nafasi bora zaidi ya kucheza."
"Ikiwa nitajitahidi kucheza vyema nikiwa Chelsea, huenda nikapata nafasi katika timu."






Hazard awapo uwanjani shughuli yake ni pevu kama inavyoonekana pichani amekusanya Vijiji

Hazard alikuwepo katika kikosi kilichoshinda ligi wakati Lille ilipopata ubingwa mwaka 2010-11 na katika msimu wake wa mwisho, alifanikiwa kufunga magoli 21 katika mechi 48.

Katika mechi yake ya mwisho dhidi ya Nancy mwezi uliopita, alifanikiwa kupata hat-trick (magoli matatu) wakati timu yake ilipocheza dhidi ya Nancy.

Lakini alishindwa kuvuma wakati Ubelgiji iliposhindwa na England katika mechi ya kirafiki Jumamosi iliyopita.

Hiyo ilikuwa ni mara yake ya 28 kuichezea timu yake ya taifa ya Ubelgiji.

Hazard sasa ni mchezaji wa pili kusajiliwa Chelsea tangu dirisha la usajili la mwezi Januari, wa kwanza akiwa ni mchezaji wa kimataifa wa Ujerumani, Marko Marinas.