Thursday, May 31, 2012

PICHA YA SIKU (photo of the day)

SERIKALI YAIKABIDHI FAMILIA YA MAREHEMU KANUMBA "THE GREAT" Tshs MIL 10


Picture













Naibu waziri wa Habari Utamaduni Vijana na Michezo Amos Makalla akimkabidhi mama mzazi wa marehemu Steven Kanumba Kitika cha Shilingi milioni 10 taslimu ikiwa ni ubani kwa niaba ya serikali

Serikali kupitia kwa Naibu waziri wa Habari Utamaduni Vijana na Michezo Amos Makalla imemkabidhi mama wa marehemu Steven Kanumba kiasi cha shilingi milioni 10 za Kitanzania ikiwa ni ubani kwa niaba ya familia.

Akipokea ubani huo mama yake Kanumba alisema" Nashukuru sana...ingawa Kanumba hatorudi lakini nashukuru sana, Naishukuru serikali, Nashukuru vyombo vya habari, Nawashukuru wasanii..sina la zaidi nashukuru sana"

Marehemu Steven Kanumba

BALOTELLI ATOA ONYO EURO, UKILETA UBAGUZI NAKUMALIZA


Mario Balotelli akiwa kwenye mazoezi na kikosi cha timu ya taifa ya Italia

Balotelli alipokuwa akitangaza azma ya kumtoa 'ngeu' mtu yeyote atakaemkebehi na kumdharau katika michuano ya Ulaya huko Poland na Ukraine

Mshambuliaji mtukutu wa Manchester City anayechezea timu ya taifa ya Italia, Mario Balotelli amesema kuwa ataondoka uwanjani endapo ataonyeshwa vitendo vya ubaguzi wa rangi wakati wa Fainali za Euro zinazoandaliwa kwa pamoja kati ya Poland na Ukraine.

Jarida ya Shirika la Utangazaji la Uingereza, BBC, lilisema kuwa wenyeji wa Fainali za Euro wamekuwa na tabia ya ubaguzi wa rangi na UEFA imesisitiza kuwa m chezo unawez akuvunjwa endapo itatokea hali hiyo.

Mshambuliaji huyo wa Italia, Balo, 21, alisema: “Endapo mtu atanipiga kwa ndizi mtaani, ni wazi nitakwenda jela kwa sababu nitamuua.“Ubaguzi wa rangi hauna nafasi kwangu, siwezi kuuendekeza. Naamini hakutakuwa na matatizo katika Fainali za Euro, na ikitokea nitarudi nyumbani.

“Lakini tuko katika michuano ya Euro 2012, najua haiwezi kutokea.”


Balotelli, 21, alikumbana na hali hiyo akiwa na City katika michuano ya Ligi ya Europa walipocheza na Porto mapema Februari.Lakini hakupata tabu sana na alipokuwa Inter Milan mwaka 2009 aliwahi kurushiwa ndizi.

Balotelli aliiambia France Football: “Najua wanaweza kunifuata askari kuja kunikama, kwa sababu naapa, nna ninaapa kweli nitampa mtu kipigo cha sawasawa. Nitawapiga kweli. “Lakini bado nina imani hilo haliwezi kutokea.”

Tukio lingine lililotokea Italia ni wakati Balotelli alipodhihakiwa na mashabiki wa Juventus.


Alisema: “Nakumbuka vizuri na hiyo ni kwa sababu nafunga mabao. Kimsingi, watakuwa watu wazuri na hawawezi kufikiria hilo la kukufanya ukasirike. Kikubwa wanachofanya ni kukuchanganya kwa kukukebehi.
Nilijifanya sioni lolote lililotokea kwa sababu nilitaka kucheza mpira. Nilikuwa bado mdogo. Nilichokifanya ni kumwambia mwamuzi. Lakini kama ningemwambia mwamuzi asimamishe mchezo nisingefunga.”

STARS 'DHAIFU' YAWAFUATA TEMBO WA IVORY COAST, MAKALLA AWATAKA KUUDUWAZA ULIMWENGU


Naibu waziri wa Habari Utamaduni Vijana na Michezo Amos Makalla akimkabidhi nahodha wa Stars Juma K Juma hapo jana tayari kwa safari ya leo alfajiri kwenda Ivory Coast

Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Kim Poulsen amesema wanakwenda Abidjan, Ivory Coast na watawaduwaza Ivory Coast kwa mchezo wao wa kwanza kuwania kufuzu Fainali za Kombe la Dunia, 2014 zitakazofanyika Brazil.

Stars na Ivory Coast zilizopambana Mei 2010 kwenye Uwanja wa Taifa na Ivory Coast kushinda bao 1-0, zitacheza mechi yao Juni 2 ikiwa ni takribani miaka miwili, mchezo utakaofanyika kwenye Uwanja wa Houphouet Boighny ulioko katikati ya jiji la Abidjan.


Kocha wa Stars Kim Puelsen katikati, kushoto ni rais wa TFF Leodgar Tenga

Timu hiyo imeondoka leo alfajiri ikiwa na msafara wa watu 32 wakiwemo wachezaji 23 na viongozi tisa akiwemo mwandishi wa habari wa magazeti ya Mwananchi Communications Ltd.

Wachezaji hao na viongopzi waliagwa jana na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo, Amos Makalla na Kim aliwaambia wachezaji wake kwamba njia pekee ya kuweza kuaminiwa na Watanzania ni kuhakikisha wanashinda pambano hilo.

"Jana (juzi) jioni nilikaa na wachezaji nikawauliza mmoja mmoja unafahamu ni kwa nini umeitwa kwenye timu ya taifa, nashukuru kwamba walinijibu kwa usahihi kabisa.

"Ukweli ni kwamba niliwaambia wajiamini kwanza wenyewe kwa kuhakikisha ushindi unapatikana na baada ya hapo mashabiki na hata vyombo vya habari vitawaamini,"alisema Kim na kuongeza: "Lakini katika kufanikisha hili nimewasisitizia hakuna mafanikio pasipo nidhamu ya hali ya juu."

Naye Naibu Waziri wa Habari Utamaduni na Michezo Amos Makalla aliwataka wachezaji wa Taifa Stars kutoweka mawazo kwamba Ivory Coast ni Chelsea kwa kuwa ina wachezaji maarufu kama Didier Drogba na Solomon Kalou ambao wanaichezea klabu hiyo.

Pia aliwataka waelekeze akili zao katika kupapambana dimbani badala ya kuhofia hujuma za nje ya uwanja za wapinzani wao.

Mkuu wa msafara huo ni Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Soka Tanzania, TFF, Crescentius Magori na pamoja na Makamu wa Rais wa Chama cha Soka Zanzibar, ZFA, Haji Ameir Haji.

Viongozi walioambatana na timu hiyo ni Kim Poulsen na msaidizi wake Sylvester Marsh na kocha wa makipa, Juma Pondamali 'Mensar'.

Wengine ni meneja wa timu hiyo, Leopord Tasso Mukebezi, daktari wa timu Mwanandi Mwankemwa, mtaalamu wa viungo Frank Mhonda na mtunza vifaa, Alfred Chimela.

Wachezaji wa Stars ni nahodha: Juma Kaseja, Aggrey Morris, Mwadini Ally, Deogratius Munishi, Nassor Masoud Cholo, Amir Maftah, Erasto Nyoni, Kelvin Yondan, Waziri Salum, Shomari Kapombe na Juma Nyoso.

Wengine ni Jonas Mkude, Mwinyi Kazimoto, Salum Aboubakar, Shaaban Nditi, Edward Christopher, Mrisho Ngassa, Frank Domayo, Mbwana Samata, Ramadhan Singano, Simon Msuva, Haruna Moshi 'Boban' na John Boko.

CHARLES TAYLOR AHUKUMIWA "MVUA" 50 JELA



Rais wa zamani wa Liberia Charles Taylor

Rais wa zamani nchini Liberia Charles Taylor amehukumiwa miaka"MVUA" 50 jela na makahakama ya kimataifa ya uhalifu wa kivita.


Taylor akiwa mahakama ya kivita wakati akisomewa mashtaka

Mwezi jana Taylor alipatikana na makosa ya kuwaunga mkono waasi nchini Sierra Leone katika vita vya wenyewe kwa wenyewe kati ya mwaka 1991 na 2002.
Upande wa mashtaka ulitaka kiongozi huyo wa zamani kusukumwa jela miaka 80. Charles Taylor amesisitiza hana hatia yeyote na anatarajiwa kukata rufaa.

Mwandishi wa BBC aliyeko The Hague Anna Holligan anasema rufaa dhidi ya hukumu hii huenda ikachukua miezi sita. Akitoa hukumu hiyo Jaji Richard Lussick amesema dhuluma zilizotekelezwa nchini Siera Leone zilikuwa za kinyama zaidi kuwahi kushuhudiwa katika historia ya binadamu.


Taylor enzi za "madudu" yaliyomgharimu kifungo cha "nyundo" 50

Mahakama maalum ya Kimataifa inayochunguza dhuluma za kivita nchini Sierra Leone ilimpata Taylor na hatia ya makosa 11 dhidi ya binadamu ikiwemo mauaji na ubakaji.

Taylor amekuwa Rais wa kwanza kuhukumiwa kwa makosa ya vita na Mahakama ya Kimataifa tangu kesi za Nuremurgs dhidi ya watawala wa Kinazi baada ya Vita Kuu ya Pili duniani.

Charles Taylor amelalamikia upande wa mashtaka kwa kuwatisha mashahidi katika kesi dhidi yake. Rais huyo wa zamani anatuhumiwa kwa kuwapa silaha waasi na kubadilishana na almasi.

Kesi dhidi ya kiongozi huyo wa zamani wa Liberia inasikilizwa The Hague kwa hofu kwamba kufanyika kwake Sierra Leone huenda kukazua vurugu katika kanda hiyo. Taylor anatarajiwa kuhudimia kifungo chake nchini Uingereza.