Monday, May 21, 2012

CHELSEA YATWAA NDOO YA LIGI YA MABINGWA WA ULAYA


Wachezaji wa Chelsea wakiwa na mwali wa ligi ya mabingwa ulaya

Meneja wa mda wa Chelsea Roberto di Matteo alipoingia mkutano wa wandishi wa habari kwa mazungumzo ya baada ya mechi saa saba na robo usiku wa manane, akijivunia rekodi kubwa kwa meneja yeyote wa muda kuwahi kushinda, machungu ya Chelsea daima kukosa Kombe la Ligi ya mabingwa tayari yalikua yamefutwa kwa dawa nyepesi kutamka, Ushindi.
Didier Drogba alipojipanga, bila pupa,wasiwasi wala hofu na kuupiga mpira ule kumpita golikipa wa Bayern, Manuel Neuer, mwenye sifa ya kuzuia mikwaju ya penati na kuthibitisha ushindi wa 4-3 kupitia matuta, miaka mingi ya kosa kosa iliwatoka wachezaji wote,wafanyakazi na viongozi wa Chelsea.

Manager Roberto Di Matteo of Chelsea speaks to the media during a press conference at Chelsea Training Ground on May 15, 2012 in Cobham, England.
Kocha wa Muda wa Chelsea Robert Di Matteo aliyeipa ubingwa wa barani ulaya Chelsea na kuweka rekodi ya kocha wa muda mwenye mafanikio zaidi
Hili lilifuatiwa na Drogba kuvua shati lake na kulipeperusha juu ya kichwa chake kuonyesha furaha ya ushindi baada ya kukimbia kuzunguka uwanja mzima, huku Fernando Torres na David Luiz wakipanda juu ya besera la goli kuonyesha furaha yao. Wakati huo Mmiliki wa klabu hio Abramovich mwenyewe akiruka na kupiga makofi huku akiimba ikidhihirisha sura isiyoonekana kwa kawaida kwa mtu msiri asiyeonyesha hisia zake.


Drogba akishangilia baada ya kutupia kambani penati ya mwisho iliyoipa ubingwa Chelsea

Ikiwa mkwaju huo ulikua wa mwisho kwa mchezaji huyu kutoka Ivory Coast kama mchezaji wa Chelsea, pamoja na bao lake la kusawazisha lile la Thomas Mueller, basi Drogba ataondoka kwa kuweka rekodi yake binafsi.


Drogba akimiliki mpira katika fainali hiyo

Drogba mwenyewe hakuweza kuelezea bayana juu ya majaliwa yake baada ya kukabidhiwa zawadi ya mchezaji bora wa mechi hio ya fainali ya Ligi ya mabingwa barani Ulaya. Punde mkataba wake unafikia mwisho na bado hakuna matumaini ya kama ataongezewa mda.

Hatma ya Meneja wa mda Di Matteo bado haijabainika na mwenyewe alishindwa kusema ni nini alidokezewa na Abramovich walipokumbatiana kwenye ngazi kabla ya sherehe za kukabidhiwa Kombe kwa mara ya kwanza katika historia ya miaka 107 ya klabu hio.
Haikua kazi rahisi kwa Chelsea uwanjani mpira ulipochezwa katika sehemu ya uwanja ya Chelsea lakini hadi mwisho lakini waliepuka uwezekano mkubwa wa kufungwa zaidi ya mabao manne ila kutimiza ndoto ya Abramovich.



Mara pekee kwa klabu hii kushamiri katika mashindano ya Ulaya, ulikua mwaka 1971 kabla ya hata Liverpool kushinda nje ya England, Chelsea ilipoichapa Real Madrid na kujishindia Kombe la Mshindi la mwaka huo wa 1971.

Drogba, aliongoza na kua kinara, na hivyo kuandika jina lake kwa vitendo katika historia. Kipa Petr Cech amepitia kipindi kigumu wakati wa kampeni ya Ligi ya mabingwa wa Ulaya lakini mjini Munich alionyesha ukomavu kwa kuzuia mkwaju wa Arjen Robben katika kipindi cha ziada na wakati wa matuta alizuia mkwaju wa Ivica Olic.
Mwamko wa Chelsea ulianza pale alipotimuliwa Andre Villas Boas kufuatia kipigo cha 3-1 na Napoli na mrithi wake Di Matteo akageuka kua chachu ya ufanisi kwa kusababisha ushindi wa Kombe la FA na mechi kadhaa za Ligi kuu ya Premiership.


Matokeo ya Napoli yakageuka kuipendelea Chelsea na baada ya hapo kuichabanga Benfica kujishindia fursa ya kukutana na Barcelona ambayo waliweza kuishinda kwa hatua zote mbili,nyumbani na ugenini licha ya kusukumwa kwa dakika nyingi.


Sifa kubwa anastahili Roberto Di Matteo aliyechimba ndani ya bongo za wachezaji aliyewafahamu na kuamini kua wana uwezo wa kushiriki na kucheza soka kwa kiwango cha juu na kushinda.

Bila shaka wadadisi watakosoa mbinu zilizotumiwa dhidi ya Barcelona na huko Munich lakini jibu la Di Matteo ni moja tu angalia rekodi ya mwaka 2012, Mabingwa wa Ulaya ni Chelsea.

Uwanja wa Allianz Arena ambapo kipute cha fainali ya ligi ya mabingwa kilipigwa na Chelsea
kuibuka kidedea


MIPIGO YA PENATI