Thursday, May 3, 2012

BURUDANI TIME (18+)

PAPISS DEMBA CISSE ATUPIA KAMBANI GOLI LA MSIMU WAKATI NEWCASTLE IKIIADHIBU CHELSEA

Goli la msimu la Demba Cisse dhidi ya CHELSEA

Timu ya soka ya Newcastle United jana waliwaadhiri wababe walioingia fainali ya ligi ya mabingwa barani ulaya timu ya Chelsea katika mtanange wa ligi kuu ya Uingereza kwa kuigaragaza kwa magoli 2-0 katika dimba lao la nyumbani hapa naizungumzia Stamford bridge.

 Papiss Cisse Chelsea
Papiss Demba Cisse akiachia mkwaju ulioelekea moja kwa moja kwenye nyavu za Chelsea zikimuacha golikipa Peter Cech akiwa ananing'inia bila mafanikio

Katika mechi hiyo Demba Cisse alitupia kambani mara mbili ambapo dakika ya 19 alimtesa vilivyo Peter Cech wa Chelsea na dakika za nyongeza akatupia la pili na kukamilisha shughuli iliyokuwa na pilipili nyingi kwa upande wa Chelsea wakati Newcastle wakiifurahia kwa ndimu iliyokolea.