Friday, April 27, 2012

GUARDIOLA KUBWAGA MANYANGA BARCELONA

Barcelona's coach Pep Guardiola walks in the sideline during their Spanish first division ''El Clasico'' soccer match against Real Madrid at Nou Camp stadium in Barcelona April 21, 2012. REUTERS/Sergio Carmona
Pep Guardiola kocha anayetazamiwa kubwaga mikoba ya kuinoa Barcelona

Kocha wa mabingwa wa Ulaya Barcelona ambao hivi karibuni walitupwa nje katika kinyang'anyiro cha kutetea ubingwa wa klabu bingwa ya Ulaya na Chelsea, Pep Guardiola atabwaga manyanga mwishoni mwa msimu huu baada ya kufikia uamuzi wa kutoongeza mkataba wake na Klabu hiyo ya Barcelona katika ligi kuu ya Uhispania.

Rais wa Barcelona Sandro Rosell aliliambia shirika moja la Habari kuwa msimu huu ndio wa mwisho Guardiola kukinoa kikosi cha Barcelona baada ya kukataa kuongeza mkataba wake ambao unamalizika mwishoni mwa msimu huu.
Rais huyo alimshukuru Guardiola kwa kusema"Thank you for your work and your love," 
akimaanisha akhsante kwa kazi yako na upendo wako.