Tuesday, April 17, 2012

HUWEZI KUAMINI KIPAJI CHA SAUTI YA HUYU MTOTO

WIGAN YAITANDIKA ARSENAL EMIRATES


Di Santos akiipatia Wigan bao la kuongoza


Wigan ilithibitisha kuwa walipoifunga Manchester United haikuwa ajali na hawakubahatisha, walithibitisha hilo siku ya Jumatatu usiku Arsenal walipoichabanga Arsenal nyumbani 2-1. Wigan ilifanya unyama huo katika kampeni zake za kubakia ligi kuu ya Premier.
Kwa ushindi huo sasa Wigana inashikilia nafasi ya 16 katika msimamo wa ligi kuu ya Uingereza.
Arsenal ilikuwa inatafuta ushindi utakayoihakikishia kuongoza kwa pointi nane mbele ya Spurs bila mafanikio.

Thomas Vermaelen akiipatia Arsenal goli la kufutia machozi

Pamoja na kipigo hiko Arsenal bado wako katika nafasi ya tatu , nyuma ya vinara Manchester United na Manchester City.
Bao la kwanza la Wigan lilitupiwa kambani na Franco di Santo katika dakika ya saba na dakika moja baadaye Jordi Gomez akapigilia msumari wa pili
Thomas Vermaelen aliipatia timu ya nyumbani ya Arsenal bao lao moja la kufutia machozi.mpaka kipyenga cha mwisho Arsenal 1-2 Wigan Athletic.
ARSENAL 1-2 WIGAN