Thursday, March 29, 2012

FABRICE MUAMBA "AFUFUKA" WACHEZAJI NA FAMILIA ZAO WAMIMINIKA HOSPITALINI KUMJULIA HALI


FABRICE MUAMBA

Habari kutoka London Uingereza zinasema kiungo wa Bolton, Fabrice Muamba ameweza kuamka kitandani na kuzungumza na wachezaji wenzake waliokwenda kumuona hospitali.


Reo Cooker,Pratley na Davies wakitoka Hospitalini kumtembelea Muamba

"Anatia moyo na hali yake inazidi kuimarika," ilisema taarifa ya pamoja ya klabu na hospitali.

Kocha wake, Owen Coyle alisema Muamba alikuwa akiangalia mechi za ligi za mwishoni mwa wiki ikiwemo timu yake ilipoibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Blackburn.


Defoe na mama yake (Sandra) na nyuma ni dada yake (Chonte) walipomtembelea Muamba Hospitalini

"Nilikuwa nasikia raha, nilikuwa sijisikii hata kulala wakati tunaongoza kwa mabao 2-0," alisema Muamba.

Kocha huyo alikuwa katika mipango ya mechi ya marejeo ya Kombe la FA na aliwashukuru mashabiki wa Tottenham Hotspur kwa msaada wao.


Benoit Assou-Ekotto akiwatilia saini mashabiki wake alipokwenda kumjulia hali Muamba hospitalini

Bolton inarudi kwenye Uwanja wa White Hart Lane kwa ajili ya mechi hiyo iliyovunjika baada ya mchezaji huyo kupatwa na shambulio la moyo na kuanguka uwanjani.

"Tutakuwa tukikuwaza, Fabrice." Wachezaji wa Bolton walisema walipomtembelea mwenzao ikiwa ni siku chache kabla ya kurudiana na Spurs.


Essien akizungumza na waandishi wa habari nje ya hospitali alipoenda kumtembelea Muamba

Wakati wanajiandaa kwenda kumtembelea mchezaji mwenzao, Zat Knight, David Wheater na Jussi Jasskelainen walikuwa wanashindwa hata kutoka hotelini kwenda London Chest Hospital.


Shaun Wright Philips na Ashley Cole nao walijumuika Hospitalini kumjulia hali Muamba

Wachezaji wa timu hiyo walikuwa wamevalia suti za michezo, na walipanda teksi kwenda hospitali kumwona.


Nahodha wa Bolton Davie na mkewe(Emma) na mtoto wao walipomtembelea Muamba

Bolton pia walirudia kuipongeza Tottenham hasa kitengo chake cha huduma pamoja na shabiki wa Spurs, Dk. Andrew Deaner.


Shabiki akiweka mdoli nje ya Chest Hospital jijini London alikokuwa akitibiwa Muamba.

Taarifa iliishukuru Tottenham waliokuwa wakimtakia kila la kheri Muamba, waliwashukuru London Ambulance Service na wale wote waliojitolea kutoka taasisi za moyo kumsaidia Muamba.

CCM HAINA JIPYA KATIKA MAENDELEO YA TANZANIA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Dk Jakaya Mrisho Kikwete akitafakari jambo katika moja ya mikutano ya Chama Cha Mapinduzi.

CCM Kweli ni chama kilichotuletea Uhuru na kutulea lakini sasa kimepitwa na wakati linapokuja swala la teknolojia kwani karne hii inabidi tuwe na Vitu vya karne hii.
Sasa ukiiangalia CCM ni ya zamani na sera za kizamani ndio maana Viongozi wa CCM wanashindwa kuleta mabadiliko katika nchi yetu.Kwa mtazamo wa kawaida wa umasikini uliokithiri wa watanzania,migogoro na ukosefu wa huduma bora za jamii ni dhahiri CCM imeelemewa na inaonekana kushindwa kutatua ama kuleta nafuu kwa watanzania kupitia serikali yake.

Nimesikitika sana kusikia Rais wetu Dk Kikwete akikosolewa na wataalamu wa Uchumi kutoka China na Vietnam mbele ya jamii na kadamnasi,Wakosoaji  Wameshangazwa sana na mfumuko wa bei na ubinafsishwaji wa viwanda.
Ni dhahiri kuwa ubinafsishaji wa Viwanda umetupandishia gharama za maisha kwani viwanda ndio kitu pekee kingeweza kumkomboa mkulima kwa kuongeza thamani ya mazao ya kilimo ambacho asilimia 80 ya watanzania wanakitegemea, na ajira za watanzania zingeongezeka kutokana na viwanda lakini leo hii tumebinafsisha kila kitu.

Mfano mzuri ameutoa Profesa Do DucDinh wa Taasisi ya kimataifa ya uchumi ya Vietnam kuwa Vietnam hawalimi kabisa zao la korosho lakini wana Viwanda vya kubangua korosho sasa iweje Tanzania ikose viwanda vya kubanguaimesheheni hapa nchini?
Suala la mfumuko wa bei Profesa Do Ducnh anasema mwaka jana alikuja akakuta kilo ya mchele 1,200/= leo hii kilo ya mchele 2,500/= ameshangazwa sana na mfumuko huo wa bei, Kama ugali ndio chakula kikuu halafu bei ya unga ipo juu unategemea maisha yatakuwaje? lazima yawe magumu nchi zote duniani chakula kikuu huuzwa kwa bei ya chini tofauti na vyakula vingine.