Thursday, March 22, 2012

ARSENAL YAICHAPA EVERTON,VERMAELEN NI NOUMER!


Arteta na Van Pesie wakishangilia goli lililofungwa na Vermaelen(5)

Theo Walcott akipunguzwa makali na Leighton Baines wa Everton

Timu ya soka ya Arsenal jana tarehe 21 machi 2012 waliutumia vizuri uwanja wake wa Emirates uliopo jijini London kwa kuichabanga Everton bao moja kwa ubuyu(1-0).
Katika meshi hiyo ndani ya dimba la Emirates ilihudhuriwa na watu 30,330 na mchezo huo ulichezeshwa na Mason.
Arsenal ambao wanaonekana kuwa fit kwa kila mechi kipindi hiki walicheza soka la kuvutia kama kawaida yao na sio mwingine aliepeleka msiba Everton bali ni Beki anaeongoza kwa kutupia kambani Thomas Vermaelen aliposukumiza mpira wa kichwa wavuni katika dakika ya 7 ya mchezo.
Mpaka mapumziko Arsenal walitoka kifua mbele kwa goli moja la kuongoza,Kipindi cha pili kilianza kwa soka la kuvutia huku Gunners wakijaribu kuongeza bao na Everton nao wakifanya jitihada kutafuta bao japo la kufutia machozi bila mafanikio.
Japo washambuliaji wa Arsenal kama Ramsey,Rosicky na Van Persie walijaribu kuchafua hali ya hewa golini mwa Everton lakini ngome ya Everton iliyoongozwa na Baines akisaidiana na Heitinga na Distin ilikaa vyema na mpaka dakika 90 zinakamilika Arsenal ndiyo iliyoibuka mshindi.

Timu:
ARSENAL; Szczesny, Sagna, Vermaelen, Koscielny, Gibbs, Walcott, Arteta, Song, Ramsey, Rosicky, van Persie

EVERTON; Howard, Hibbert, Heitinga, Distin, Baines, Pienaar, Fellaini, Osman, Drenthe, Cahill, Jelavic.

MANCHESTER CITY YAIBOFOA CHELSEA 2-1


Golikipa wa Man City Joe Hart akichumpa bila mafanikio kuokoa mpira uliopigwa na Garry Cahill ukielekea kambani.

Aguero akitupia kambani kwa mkwaju wa penati na kuisawazishia Man City

Nasri akitupia kambani na kuandika bao la pili na la ushindi kwa Man City,Cech hoooooi

Manchester City imeendeleza kampeni zake za kuusaka ubingwa wa Ligi kuu ya Uingereza pale ilipoichabanga timu ngumu ya Chelsea kwa kamba 2-1 mchezo uliopigwa katika dimba la Etihad jijini Manchester.Mchezo ulipigwa jana tarehe 21 march 2012 ukichezeshwa na refa mahiri Dean.

MAN C 2-1 CHELSEA
Katika kipute hiko iliwachukua takriban dakika 60 mashabiki waliohudhuria mtanange huo kushangilia bao na bao hilo likitiwa kambani na Garry Cahill na kuifanya Chelsea kuongoza mchezo huo uliokuwa wa kawaida tofauti na ulivyotegemewa na wengi.
Mbwembwe za mashabiki na wachezaji wa Chelsea za kuongoza zilikomeshwa katika dakika ya 78 pale refa Dean alipoizawadia mkwaju wa penati Man City na bila ajizi wala kokoro mkwaju huo ulitiwa kambani na Sergio Aguero na kubadilisha taswira ya mchezo na kusomeka 1-1.
Zikiwa zimesalia dakika 5 ili kila mshabiki alielipia mechi hiyo kuhesabu maumivu kwa kuona mchezo wa sare Vijana wa Manchini walikaza na kufanikiwa kuwanyanyua vitini mashabiki wa Man City huku wakiwaonesha milango ya kuondokea wale wa Chelsea, kwa goli kali na la kuvutia lililotupiwa kambani na Mshambuliaji mzuri wa sura na uchezaji Samir Nasri katika dakika ya 85.
Bao hilo la Nasri lilionekana kuwachanganya Chelsea hasa kocha wao wa kuunga unga De Matteo na kushindwa kukaa kwenye benchi akiwahimiza kina Drogba kufanya mambo bila mafanikio yeyote na mpaka dakika 90 zinakwisha ni Man City ndio walioibuka kidedea na kuwaacha Chelsea walikwa wamelowa ndembendembe kama laki si pesa.
Vikosi vilikuwa hivi;

MAN CITY; Hart, Zabaleta, Richards, Toure, Clichy, Silva, Toure Yaya, De Jong, Nasri, Aguero, Balotelli

CHELSEA; Cech, Ivanovic, Luiz, Cahill, Cole, Mikel, Meireles, Ramires, Lampard, Mata, Torres