Friday, March 16, 2012

MAN U YACHEZESHWA UKUTI NA ATHLETICO BILBAO YACHAPWA KINOMANOMA


Golikipa De Gea akichumpa bila mafanikio na kuruhusu mpira uliopigwa na Llorente kutinga wavuni na kuandika bao la kwanza kwa Athletico Bilbao.

Manchester United jana ilipokea kipondo cha kufa mtu kutoka kwa timu ngumu ya Uhispania Athletico Bilbao cha kamba 2-1.
Katika mchezo huo wa 16 bora ya ligi ya mabingwa sio mwingine bali ni Llorente aliyeanza kutupia kambani kwa shuti kali lililomuacha hoi golikipa wa Man United De Gea akichumpa bila mafanikio na kuipatia Athletico Bilbao bao la kuongoza katika dakika ya 23.
Ngozi iliendelea kusukumwa na kwa mara nyingine tena De Marcos katika dakika ya 65 aliinyong'onyesha Man United na kuwalaza unono mashabiki wa Man U kwa kutupia kambani bao la pili.

Wachezaji wa Man United wakishangilia goli la Rooney.

Goli 2-0 zilidumu mpaka kipindi cha kwanza kinamalizika na timu zote kwenda vyumba vya kupumzikia huku Man U wakiwa vichwa chini na Athletico Bilbao wakiingia vyumbani vifua mbele.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi huku Bilbao wakionekana kuridhika na goli mbili na kuanza kulinda,soka lilipigwa kiasi cha mashabiki wa Man United kuanza kuachia viti na kutafuta milango ya kutokea..hamad mungu sio Athumani,alikuwa ni mchezaji kipande cha mtu Wayne Rooney katika dakika ya 80 alipofanikiwa japo kutikisa nyavu na kuipatia Man United bao la kufutia machozi na kuwarudishia uhai mashabiki wa Man United waliokuwa wakipumulia mipira kwa dakika zote 80.
Man United 2-1 Athletico Bilbao