Thursday, March 15, 2012

MAMA AJERUHI MWANAWE KWA MPIRA

Video hii inaonesha tukio lililotokea huko majuu ambapo mtoto alikuwa akicheza mpira katika bustani ya nyumbani kwao, mama kwa upendo akaona akajiunge na mwanae katika kucheza lile kabumbu.
Wakati mama na mwana wakirukaruka huku na kule wakisukuma lile kabumbu kwa muda fulani kama kawaida kitu chochote hasa michezo ukiufurahia sana mzuka unapanda si kitoto,balaa lililotokea baada ya mama na mwana kupandwa na mzuka wa soka ni mama kujikuta akifumua shuti la kwelikweli kuelekea kwa mwanawe na kwa bahati nzuri au mbaya mama alifumua shuti lililokwenda moja kwa moja kwenye uso wa mwanawe kama unavyoona wachezaji wanapofumua mashuti na kutinga wavuni basi ndivyo ilivyokuwa.
Mtoto ilibidi aangue kilio baada ya shuti kutua sawasawa katika paji la uso wake, mama alipatwa na kazi ya ziada kumnyamazisha mtoto na hatimae mtoto alinyamaza na kama ilivyo kawaida kwa watoto hawana kinyongo muda uleule akatabasamu na akaanza tena kucheza mpira huku akimuita mama yake, safari hii mama alikuwa kama kafungwa mawe miguuni alishindwa kabisa kupiga mpira.