Friday, March 9, 2012

WENGER AOPOA "JEMBE" KUTOKA F.C COLOGNE

Lukas Podolski
Kifaa kipya kitakachotua Arsenal Lukas Podolski

Klabu ya Arsenal imeafikiana na mshambuliaji wa Ujerumani Lukas Podolski kutoka klabu ya Cologne, BBC Michezo imefahamu.
Kwa mujibu wa taarifa Arsenal italipa pauni za Uingereza £10.9m kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 kwa mkataba wa miaka minne akilipwa pauni £100,000 kila wiki.