Monday, February 27, 2012

Liverpool mabingwa Carling Cup baada ya ukame wa miaka 6

Cup of joy: Gerrard lifts lifts the Carling Cup trophy as Liverpool celebrate
Liverpool wakishangilia ubingwa wa Carling

Ilikuwa fainali ya kukata na shoka iliyochezwa kwa muda wa dakika 120 baada ya kukosa mbabe ndani ya dakika 90 na hatimaye mshindi alipatikana kutokana na mikwaju ya penati.

Bright start: Cardiff's Joe Mason casually rolled his side into the lead in the first half
Joe Mason akitia "kambani" goli la kuongoza dhidi ya Liverpool

Comeback: After plenty of near misses, Liverpool hit back through Martin Skrtel
Martin Skrtel akiisawazishia Liverpool dakika ya 60

Ni miaka sita tangu kuwe na ukame wa vikombe kwa Liverpool na sasa wamekinyaka cha Carling. Mpambano ulianza kwa kasi na Cardiff ndio walikuwa wa kwanza kutikisa nyavu za Liverpool goli likifungwa na Joe Mason, lakini Liverpool walijibu mapigo na kujipatia goli la kusawazisha kwa bao lililofungwa na Skrtel dakika ya 60.

Liverpool vs Cardiff

Hadi dakika 90 za kawaida zinamalizika timu hizo zilitoshana nguvu na mwamuzi wa mpambano huo  kulazimika kuongeza dakika nyingine 30.

Super sub: Kuyt scored within five minutes of coming on
Dirk Kuyt muuaji wa goli la pili

Katika kipindi cha pili cha dakika za nyongeza Mshambuliaji wa Liverpool Dirk Kuyt, alieingia kuchukua nafasi Andy Carrol alitia kambani na kuipatia Liverpool goli la pili katika dakika ya 108.
Vijana wa Cardiff hawakukata tamaa na zilipotimia dakika 118 mchezaji Ben Turner wa Cardiff alizima ndoto za Liverpool kuibuka mabingwa ndani ya dakika 120 baada ya kutupia kambani baada ya kizaazaa kutokana na kona iliyoelekezwa langoni mwa Liverpool.
Dramatic scenes: Ben Turner took the game to penalties
Ben Turner akitia kambani baada ya kizaazaa kutokea langoni mwa Liverpool kutokana na Kona
Atmospheric: Liverpool fans held a protest inside the ground against the launch of the Sun on Sunday
Mashabiki wa Liverpool

Baada ya dakika 120 kukamilika ndipo changamoto ya mikwaju ya penati ilipofikia ambapo Liverpool walifanikiwa kufunga penati 3 zilizotiwa nyavuni na Dirk Kuyt, Glen Johnson na Downing. Waliokosa ni Steven Gerrard na Charli Adam.

Timu ya Cardiff walifanikiwa kutia nyavuni penati mbili zilizopigwa na Don Cowie na Wittingham, na wachezaji waliokosa penati ni Kenny Miller, Rudy Gestede na Anthony Gerrard.
Magic moment: Liverpool's players rush to celebrate their win
Wachezaji wa Liverpool wakishangilia ubingwa baada ya binamu yake Steven Gerrald,Anthony Gerrald kukosa penati ya mwisho ya Cardiff.

Arsenal nomaaaa,yaibanjua Spurs 5-2


Thomas Rosicky akishangilia "kamba" ya tatu dhidi ya Spurs

Matokeo ya mwisho katika mechi kati ya Arsenal na Tottenham Hotspurs yalisomeka 5-2, Magoli ya Arsena yakifungwa na Sagna, Van Persie, Rosicky, Walcott*2. huku Saha na Adebayor wakiipatia Spurs mawili ya kufutia machozi. Mechi hiyo ilipigwa katika dimba la Emirates ambapo mashabiki wa Arsenal walishuhudia timu yao ikitoka nyuma kwa magoli mawili na kupata ushindi wa kishindo dhidi ya Spurs.

Robin Van Persie,Walcott na Chamberlain wakishangilia goli la nne

MUGABE ATIMIZA "NYUNDO" 88

Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe
Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe

Sherehe za kuadhimisha Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe kutimiza umri wa miaka 88, zimefanywa katika mji wa Mutare, mashariki mwa nchi, na maelfu ya watu wamehudhuria.
Matawi ya chama cha ZANU PF cha Rais Mugabe, yalichanga kugharimia sherehe hizo ambazo piya zilikuwa na mashindano ya warembo na mechi ya mpira.
Aliwaambia wafuasi wake kwamba wale wanaopinga msimamo wake dhidi ya wapenzi wa jinsia moja na ndoa kati yao, wapotelee mbali.
Bwana Mugabe alikanusha kuwa ni mgonjwa, na mapema juma hili alisema yeye kakazana kama kigongo na anaweza kuongoza nchi..
Umri wake pamoja na taarifa kuwa Rais Mugabe anauguwa saratani ya kibofu, imezusha wito mwengine kuwa Zanu PF inafaa kubadilisha uongozi.
Lakini chama chake kimemuunga mkono agombee tena urais mwaka huu.