Friday, February 24, 2012

MAN UNITED CHUPUCHUPU EUROPA

Manchester United iliponea chupuchupu kufungwa na Ajax ya Uholanzi katika uwanja wa nyumbani wa Old Trafford.
Javier Hernandez
Chicharito akitupia kambani bao la kufutia machozi wakati Man U ilipofungwa na Ajax licha ya kufuzu kuendelea kucheza Europa

Bao la Toby Alderweireld liliwalazimu kukubali kushindwa katika mechi hiyo ya Europa iliyochezwa Alhamisi jioni.
Licha ya hofu iliyosababishwa na Ajax, Man United ilifuzu kuwa miongoni mwa vilabu 16 ambavyo vitaendelea kucheza katika ligi hiyo ya Europa.
Sasa Man U inatazamiwa kukutana na Athletic Bilbao ya Uhispania
Lakini kutokana na wingi wa mabao, Man U ilifuzu kwa jumla ya magoli 3-2.
Ajax awali ilikuwa imeangamizwa kwa bao la awali la Javier Hernandez, baada ya kugongewa mpira vyema na Dimitar Berbatov.
Ingawa Man U wako njiani kuelekea kwa fainali Bucharest, ambako fainali itafanyika, kushindwa kwa timu hiyo kuliondoa matazamio mengi ya mashabiki, baada ya meneja wa muda wa timu ya England, Stuart Pearce, kuwachagua wachezaji sita kutoka Old Trafford, na ambao ni miongoni mwa wachezaji 25 watakaopambana na Uholanzi, Jumatano ijayo, katika mechi ya kirafiki.


Pearce alikuwepo uwanjani kutizama namna wachezaji wanne, kati ya hao sita, wakicheza; Tom Cleverley, Chris Smalling, Ashley Young na Phil Jones.
Licha ya kwamba Man U ilikuwa imeishinda Ajax, mabingwa mara nne barani Ulaya, walipokutana katika mechi yao ya awali, meneja Sir Alex Ferguson hakutaka utani katika mechi ya Alhamisi.

Man City kiboko,Inter Milan na Bayern Munich "Ndembendembe"


                       Man city 4-0 Porto

MABINGWA watetezi wa Europa Ligi, Porto wamevuliwa ubingwa huo baada ya kuchakazwa 4-0 na Manchester City na kuondolewa kwa jumla ya mabao 6-1 na vinara hao wa Ligi Kuu ya England juzi Jumatano.

Walifungwa 2-1 nyumbani hivyo timu hiyo ya Ureno ikawa na matumaini ya kurekebisha makosa ili iweze kusonga mbele kwa hatua ya 16 bora, lakini walipata pigo sekunde ya 19 kwenye Uwanja wa Etihad kwa bao la kuongoza la City lililofungwa na Sergio Aguero.

Katika usiku huo ambao kocha Roberto Mancini alisema mshambuliaji wake mtukutu Carlos Tevez amerejea baada ya kuwa nje kwa wiki kadhaa kufutia uamuzi wake wa kuomba radhi kwa kitendo cha kugomea kucheza, Aguero alionyesha kiwango cha juu na kuthibitisha kuwa City ina washambuliaji makini hata asipokuwepo Tevez.

Alitegeneza bao kwa mshambuliaji Edin Dzeko aliyeingia baada ya dakika ya 76 wakati City ilipoisambaratisha Porto.Pia bao la David Silva na David Pizarro yalikamilisha kalamu ya timu hiyo ya Mancini na kujikatia tiketi ya kufuzu kwa hatua ya 16 bora ya michuano hiyo.

Porto walimaliza pungufu mchezo huo baada ya Rolando kuonyeshwa kadi ya njano ya pili kwa kumfokea mwamuzi akipiga bao alilolifunga Dzeko.

MARSEILLE, Inter Milan wamehadhibiwa kwa mbinu zao mbovu wakati Andre Ayew alipofunga kwa kichwa bao pekee na kuipa Olympique Marseille ushindi 1-0 kwenye mchezo huo wa kwanza wa Ligi ya Mabingw hatua ya 16 bora.

Ayew alifunga bao hilo akiunganisha kwa kichwa mpira wa kona uliopigwa na Mathieu Valbuena katika dakika tatu za nyongeza na kuwaacha wachezaji wa Inter wakitikisa vichwa wasiamini kilichotokea.

Kocha wa Inter, Claudio Ranieri alimweka benchi mshambuliaji wa Argentina, Diego Milito, pamoja na kuwa huyo ndiye mchezaji pekee aliyeifungia timu hiyo katika michezo saba iliyopita, ukiwe ule aliofunga mabao nne walipotoka sare ya 4-4 na Palermo katika Serie A wiki tatu zilizopita.

Wesley Sneijder na Mauro Zarate hawakuwa kwenye kiwango kizuri dhidi ya Marseille, lakini Milito hakuingizwa na Ranieri alipotumia wachezaji wawili wa akiba kati ya watatu huku Giampaolo Pazzini pia alibaki benchi.

“Milito alikuwa na mafua wiki hii. Sikutaka kuhatarisha afya yake,” alisema Ranieri.Ranieri anaonekana anataka kujipanga kwa ajili ya mchezo wa marudiano utaofanyika nyumbani kwao San Siro hapo Machi 13.

BASEL, Timu ya Basel imepiga hatua moja kubwa katika Ligi ya Mabingwa baada ya kuidungua Bayern Munich kwa bao 1-0 na kujiweka vizuri kwenye harakati zake za kufuzu kwa robo fainali.

Mshambuliaji Valentin Stocker aliyeingia akitokea benchi alifunga bao hilo la ushindi kwa mabingwa hao wa Uswisi dakika ya 86 kwa shuti lililompita tobo kipa wa Bayern, Manuel Neuer.

Bayern walikosa mara mbili kwenye mchezo huo wakati mashuti ya Aleksandar Dragovic na Alexander Frei yalipogonga mwamba na kutoka, timu hiyo ya Uswisi ambayo mfumo wake wa kushambulia kwa kushtukiza ndio uliowamaliza Manchester United kwenye hatua ya makundi.

Hilo ni pigo jingine kwa Bayern ambao wamekuwa kwenye kiwango cha chini kwenye Bundesliga wakiwa nyuma kwa pointi nne kwa vinara Borussia Dortmund

STARS D.R.C HAKUNA MBABE

Timu ya mpira wa miguu ya Tanzania (TAIFA Stars) imeshindwa kutumia uwanja wake wa nyumbani kwa kukubali kulazimishwa suluhu na DR Congo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.Mchezo huo wa kirafiki wa kimataifa ulitoa nafasi kwa makocha wa timu zote kuangalia ubora wa vikosi vyao kabla ya kucheza mechi zao za kuwania kufuzu kushiriki Kombe la Mataifa ya Afrika 2013.

Taifa Stars itawakaribisha Msumbiji kwenye uwanja huo Jumatano ijayo katika kampeni yake ya kusaka tiketi ya kwenda Afrika Kusini.

Stars ilianza mchezo huo kwa taratibu na kuwaruhusu DR Congo kufanikiwa kufika langoni kwa Taifa Stars mara mbili ndani ya dakika 5, kupitia kona ya Mutombo na mpira wa adhabu wa Kasusula Kilisho uliogonga mwamba na kutoka baada ya Tresor Mputu kufanyiwa faulo na Stephano Mwasika.

Katika mechi hiyo nahodha Shadrack Nsajigwa nusura amchape makofi mshambuliaji Hussein Javu baada ya kupiga shuti hafifu akiwa yeye na kipa Bolongo kwenye mchezo huo ulioshudiwa na mashabiki wachache wa Tanzania, pia kulikuwa na kikundi cha mashabiki kutoka DR Congo.

Stars walijitahidi kutawala mchezo huo, lakini Congo inayoundwa na nyota wengi wa TP Mazembe walionekana kumiliki vizuri zaidi sehemu ya kiungo, ila washambuliaji wake walikosa umakini kwenye umaliziaji.

Katika dakika ya 22 kipa Juma Kaseja alifanya kazi kubwa ya kumzuia Deo Kanda asifunge baada ya mshambuliaji huyo kuwatoka mabeki wa Stars na kupiga shuti la pembeni vilevile dakika ya 24 Mwasika aliushika mpira katika harakati za kuokoa na mwamuzi Israel Mujuni aliamuru faulo iliyopigwa na Kasusula na kutoka nje.

Ngome ya Stars ikiwa chini ya Agrey Morris, Juma Nyoso, Nsajigwa na Mwasika katika kipindi cha kwanza ilikuwa imara na kucheza vizuri ili kuhakikisha wanawazuia vilivyo washambuliaji wa Wakongo.

Mshambuliaji Mrisho Ngasa alifanya juhudi binafsi katika dakika ya 32, ambapo alipiga shuti la mbali la mita 35, lakini shuti hilo lilipaa juu kidogo ya goli la DR Congo.

Pia John Boko alijitahidi kufunga baada ya kutuliza mpira vizuri na kupiga shuti kali akiwa nje ya 18 katika dakika ya 45, ambapo shuti lake lilipaa sentimita chache kwenye lango la Congo.

Mwanzoni mwa kipindi cha pili kocha wa DR Congo, Claude Le Roy alimpumzisha kipa Bolongo na kumwingiza Kidiaba Muteba wakati Jan Poulsen aliwatoa Ngasa, Kaseja, Javu na Nsajigwa na kuwaingiza Mwadini Mwadini, Said Nasoro, Uhuru Selemani na Nsa Job.

Dakika ya 56, kipa Mwadini alithibisha ubora wake kwa kuokoa kwa ufundi mkubwa mpira wa kichwa uliopigwa na Kayiba, ambapo Stars ilijibu mapigo dakika moja baadaye baada ya Boko kujirusha vizuri kujaribu kufunga kwa kichwa krosi iliyopigwa na Abdi Kassim.

Kocha Poulsen alifanya mabadiliko mengine katika dakika ya 58 kwa kuwatoa Mwinyi Kazimoto, Kassim na kuwaingiza Jonas Mkude na Abubakar Salum 'Sure Boy' nao Congo waliwatoa Mputu na kumwingiza Amomo Ngoy.

Pamoja na makocha wote kufanya mabadiliko hayakuweza kuwasaidia kwani hadi filimbi ya mwisho inapulizwa na mwamuzi Mujuni matokeo yakulikuwa suluhu.