Monday, January 23, 2012

Bob Junior apiga show nyumbani kwa "jimama" alipwa milioni 7

Msanii wa bongo fleva ambaye ni muimbaji na mtayarishaji wa muziki (Producer) na anajulikana kama Rais wa wasafi,rais wa masharobaro,shombeshombe hivi karibuni alipiga show nyumbani kwa mama mmoja mwenye mahela ya kufa mtu na kulipwa pesa taslimu shilingi za kitanzania milioni 7 bila punguzo,hapa namzungumzia Raheem Rummy Nanji a.k.a Bob Junior.


Raheem Nanji a.k.a Bob Junior katika moja ya show zake

Katika mahojiano ya Bob Junior na radio moja jijini Dar es salaam alifunguka na kuelezea jinsi ilivyokuwa. "Aaah mimi nilipewa issue kuwa kuna mama anahitaji ukapige show maeneo ya Masaki nikakubali kwa malipo ya milioni 5" Alisema Bob Junior.
Huku akitegemea labda akifika atakuta nyomi la watu wakimsubiri atoe show, Bob Junior alishangaa kuingia kwenye nyumba ya jimama lililoshiba pesa huku mama huyo akiwa peke yake,"Nilipofika nyumbani kwake nilishangaa yupo peke yake,nikamuuliza nitafanyaje show? mama akajibu we fanya show usijali".alisema Bob Junior.

Kutokana na mshtuko jimama lilimtolea uvivu Bob Junior na kumuuliza unataka kiasi gani? tofauti na mapatano ya awali safari hii Bob Junior akataka alipwe shilingi milioni 7, bila ajizi mama akakubali kutoa dau la milioni 7 ili apate show huku akiwa peke yake hapo katika "bangalow" lake.

Baada ya mama kukubali kutoa milioni 7 Bob Junior alianza kutoa show."Kweli nilipiga show huku mama akiwa peke yake, kwanza nilipiga sebene la dakika kadhaa yaani mama alicheka sanaaaa" alisema Bob Junior.
Mtangazaji wa radio hiyo alipotaka kujua kama baada ya show mama hakumpa usumbufu mwingine? Bob Junior alifunguka kama ifuatavyo,"Hamna kitu mimi baada ya kupiga show nikatambaa,mimi pale nilienda kikazi nilipopata changu nikatambaa,au nimefanya vibaya?" Bob Junior alimuuliza mtangazaji.

Man City kiboko, Man United yairarua Arsenal

Manchester United imezidi kuipa shinikizo Manchester City iliyo kwenye kilele cha Ligi kuu ya England kufuatia mkwaju wa Danny Welbeck dakika chache kabla ya mechi kumalizika.
Mwanzoni mwa mechi hii United ilikua nyuma kwa pointi sita baada ya Manchester City kuirarua Tottenham hotspurs 3-2 kwenye uwanja wa Ettihad mapema siku ya jumapili.
Man City ipoiadhibu Tottenham.

Manchester United iliongoza kwa bao la Antonio Valencia dakika moja kabla ya kipenga cha mapumziko kuipa klabu yake bao 1-0. Bao hilo lilifutwa na la nahodha wa Arsenal katika kipindi cha pili na kuonekana kama liliowaamsha wachezaji wa Arsenal.
Mabadiliko yaliyofanywa na pande hizi mbili hayakuonekana kubadili mchezo ingawa wadadisi wengi wanajiuliza sababu iliyomfanya Arsene Wenge kumuondoa mchezaji wake aliyeonyesha mchezo mzuri Alex Oxlade-Chamberlain.
Arsenal ilipolambwa na Man United
Licha ya juhudi na kuonyesha matumaini ya kuongezea mabao kwa Arsenal Manchester United ikitumia uzowefu wake na kuzingatia mpango wake waliokuja nao waliendelea kuizuia Arsenal isifurukute na kama ilivyo tabia yao ya kukamilisha tamaa yao dakika za mwisho,zikisalia dakika tisa kabla ya kumalizika kwa mechi Danny Welbeck akatikisa nyavu za Arsenal na kuipatia ushindi na pointi tatu. Arsenal 1 Manchester United 2.