Wednesday, December 7, 2011

Nusu fainali CECAFA ni Kilimanjaro Stars vs Uganda,Sudan vs Rwanda

Uganda itamenyana na wenyeji Tanzania Bara katika nusu fainali ya Kombe la Cecafa siku ya Alhamisi, baada ya timu zote mbili kushinda katika mechi za robo fainali siku ya Jumanne mjini Dar es salaam.
Uganda Cranes waliishinda Zimbabwe 1-0 katika mechi ya kwanza, nao Kilimanjaro Stars wakawafurahisha mashabiki wa nyumbani kwa kuifunga Malawi 1-0 katika robo fainali ya mwisho.
Bao lao la Tanzania Bara la ushindi lilifungwa na Nurdin Bakari katika dakika ya 35, kwa kukamilisha pasi kutoka Mrisho Ngasa.
Tanzania Bara ndio mabingwa watetezi wa kombe hilo.
Zimbabwe waliudhibiti mchezo dhidi ya Uganda lakini wakakosa bahati ya kufunga.
Hamis Kiiza ndiye aliyefungia Uganda bao hilo moja.
Nusu fainali nyingine siku ya Alhamisi itakuwa kati ya Sudan na Rwanda.