Thursday, November 3, 2011

Wimbo wa leo, Moyo wa Subira-LINEX

Man U, Man C, Real, Bayern, Ajax, Zafanya kweli ligi ya mabingwa ulaya

Yaya Toure akishangilia goli.

Wakati Man United wakisumbuliwa na na Otelul Galati, mahasimu wao Man City walikuwa wakiwafunza mpira Villareal nyumbani kwaoUhispania.

Yaya Toure aliipatia Manchester City magoli mawili na kuiongezea matumaini ya kusonga mbele katika michuano hiyo ya klabu bingwa bara Ulaya.

Ingawa Man City walikuwa wanacheza kama watu walio uwanjani kwao wakifanya mazoezi ,lakini walitoka uwanjani wakiwa na hofu baada ya mchezaji wao matata David Silva kuondoka uwanjani akiwa na maumivu mgongoni.

Olympique Lyon 0-2 Real Madrid

Cristiano Ronaldo alifunga mabao mawili na kuipatia Real Madrid ushindi wa mabao mawili na wenyeji wao Olympique Lyon ya Ufaransa sufuri.

Ajax Amsterdam 4-0 Dynamo Zagreb.

Nayo Ajax Amsterdam iliwachapa wageni wao Dynamo Zagreb 4-0 .

Hivyo Real Madrid wanaongoza kundi D na pointi 12 wakifuatwa na Ajax Amsterdam na alama 7.

Bayern Munich 3-2 Napoli.

Bayern Munich waliwafunga wageni wao Napoli ya Italy 3-2.

Kwa ushindi huo Bayern iko kileleni mwa kundi A na pointi 10 wakifuatwa na Manchester City na pointi 7. Villarreal ni ya mwisho.

Manchester United waliwafunga Otelul Galati mbili sufuri lakini walitolewa jasho na timu hiyo ya Rumania.
Antonio Valencia aifungia Man U bao la kwanza
Wakati Antonio Valencia alipoifungia Man U bao la kwanza katika dakika ya nane , mashabiki wa mashetani wekundi walikuwa na matumaini makubwa kuwa timu ya Otelul ingelibebeshwa gunia la mabao. kumbe sivyo!
Baada ya bao lao la kwanza, vijana Sir Alex Ferguson ambao walikuwa wanacheza nyumbani Old Traford hawakuwa na mchezo wa kuvutia.
Ni baadae sana katika dakika ya 87 ambapo Wayne Rooney aliifungia Manchester United bao la pili.
Hii ilikuwa ni mara yakwanza kwa Man U kucheza katika uwanja wao wa nyumbani tangu walipopigwa 6-1 na jirani zao Man City.
Tangu kipigo hicho Manchester United hawaja weza kutulia na kuonyesha mchezo wa kuvutia. Hata hivyo la muhimu nikuwa Jumatano usiku waliifunga Otelul Galati, 2-0 na kuzoa pointi tatu.
Baada ya matokeo ya mechi hizo Manchester sasa wanaongoza kundi C na point nane sawa na Benfica ya Ureno lakini kwa wingi wa magoli.