Tuesday, November 1, 2011

Rangi nyeupe ni mchanganyiko wa rangi zote saba

Kwa wale ambao mmesahau kidogo Geography napenda kuwakumbusha kuwa Unapokuwa na rangi zote saba ukazichanganya ndipo unapopata rangi nyeupe, kuanzia sasa kaa ukielewa kuwa karatasi nyeupe ni muunganiko wa rangi zote saba katika mboni za macho yako.

Hotuba ya Obama muda mfupi baada ya kuukwaa u-presidaa(Nigga Version).....Obama The Nigga

Obama the Nigga...

Niggaz, bitches and all mother fuckers, this is the real shit right here! They said no black ass nigga is gonna do this presidential shit. They said we dont have the juice, or the kind of shit needed to run this government shit. They beat our asses down, broke the spirit of true mother fuckers but today, I stand here and say, we run this f**king show! This is the shit we can believe in!

I know some of u niggaz think this shit was easy. Men, I have to tell you it freaking wasnt. I had to beat Clinton 's ass, and beat one silly old bastard called McCain. Telling lies on me, spoiling my reputation. Thats no way to treat a nigga! But him. He aint gonna mess with no niggaz like me no more. We ran his ass down all over this country!

To the outgoing head nigga, Bush, no love lost bro! You are one dumb-ass mother fucker, but you are stll cool bro!

To these freaking terrorists, ... Osama ... am'a hunt your ass down, spray it with ketchup and beat it with a freaking hot rod you son of a gun! You dont land here and think you can smoke us to death. We gonna smoke yah out! Am sending the specialized G-Unit to deal with ur crooked ass. Fifty and ur crew, teach that sucker how to treat a nigga!

To my father, dudes, that nigga was the illest in the land. At a time when they couldnt serve a nigga coffee in America , this nigga was busy getting some from a white lady! Guy got game I tell bros. He had her lickin and singing to his tune in no time. He did it like a true nigga and thus America , here I stand. The fruit of a true black ass nigga!

To other Presidents all around the world, if u are corrupt, am gonna smoke ur ass! If you dont want to end conflict, am gonna smoke your ass! If you steal from your country, am gonna smoke your ass. If u make fun of me, your ass is coming down! If you are Robert Mugabe, am gonna smoke your ass nigga! Change your name so I dont find u. Am gonna give you shit to believe in, NIGGA!

And I understand the financial shit the country is in is the size of your momma's ass! But let me iron it out for you. Am gonna get into that freaking financial building with an AK-47 until those white ass experts solve the crisis else am gonna smoke their asses too! What do they mean they cant solve it. They are white! They supposed to be all genius and all. They understand this shit better than a nigga! So they have two options. Solve it or SOLVE IT! Dumb-ass whites!

To wind up, lets remember those who were part of the struggle. Martin Luther King, Tupac Shakur, Biggie and Michael Jackson. That last nigga aint dead but his a** truly aint gonna last long!
Yow Nigga! Its time I gonna get ma black ass back in the white house!!
God bless America !

Kivazi cha leo

Mwanadada aliejulikana kwa jina moja tu la Elly akiwa ndani ya duka moja jijini Atlanta, akiwa ametinga kivazi kilichowaacha wengi kwenye mshangao huku yeye akiwa hana habari...nimeipenda hiyo.

MIAKA 50 YA UHURU-MWL NYERERE AKIHUTUBIA SIKU YA WAFANYAKAZI 1995

Hayati baba wa Taifa Mwl Julius Kambarage Nyerere akihutubia Taifa katika maadhimisho ya siku ya wafanyakazi mwaka 1995

MATONYA ANAMILIKI HOTELI YENYE THAMANI YA SHILINGI MILIONI 150


Seif Shabaan a.k.a MATONYA

Mwanamuziki Nguli katika sanaa ya Tanzania ya muziki aina ya bongo flavour Seif Shaaban maarufu kwa jina la Matonya hakika anaweza kuwa mfano wa miongoni mwa wasanii wenye mafanikio hapa Tanzania "BONGO".
Matonya aliyeanza muziki mwaka 2000 na wimbo wake wa kwanza kuuachia ulikuwa ni uaminifu mwaka 2001.
Matonya ambaye mbali na muziki ni mfanyabiashara ya magari kutoka nje amefanikiwa kwa kiasi kikubwa na hivi sasa anamiliki hoteli yenye thamani ya shilingi milioni 150 za kitanzania.
Hoteli hiyo ipo Tanga mjini mtaa wa White Rose na inatarajiwa kufunguliwa miezi michache ijayo. hongera sana Tonya boy..

SIMBA S.C KULIPIZA KUMALIZA HASIRA KWA MORO UNITED KESHO?

Timu ya Simba inayoongoza ligi kuu Tanzania bara wana nafasi kubwa ya kupoza moto unaoendelea kufukuta kwenye jeraha la kichapo cha bao 1-0 toka kwa mtani Yanga Jumamosi iliyopita, lakini iwapo tu watatumia dakika 90 kupata ushindi katika mechi yao kesho ya kufunga duru la kwanza dhidi ya Moro United kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Kocha wa Simba Mganda, Moses Basena alikitupia lawama kikosi chake, hasa safu ya ushambuliaji akilaumu kwa matumizi mabaya ya nafasi nyingi za kufunga walizopata bila kutumia kwenye mechi dhidi ya Yanga.

Lakini jana alisema kikosi chake kipo kwenye hali nzuri na tayari ameshafanya marekebisho kadhaa yaliyotokana na mapungufu ya mechi iliyotangulia."Kikubwa kwetu ni kushinda mchezo huo na kufikisha pointi 30 katika mzunguko huu wa kwanza wa Ligi Kuu," alisema Basena.

"Nafikiri tutakuwa tumejiweka kwenye nafasi nzuri ya mbio za kutwaa ubingwa wa ligi msimu huu," aliongeza.Alisema haoni sababu ya kukumbuka kufungwa na Yanga isipokuwa akili yake kwa sasa ameiweka zaidi kwenye mbio za kutwaa ubingwa wa ligi.

"Nimewataka wachezaji kutulie na kusahau yaliyowapata Jumamosi iliyopita na kuweko akili na nguvu kwenye mchezo wa kesho dhidi ya Moro United," alisema Basena.Naye kocha wa Moro United, Hassan Banyai alisema wamejipanga vizuri kuhakikisha wanaishinda Simba kwenye pambano na kujiweka katika nafasi nzuri kwenye msimamo wa ligi hiyo.

"Nashukuru kurejea kwa beki wangu wa kati ambaye alikuwa anatumikia adhabu ya kadi, Tumba Sued," alisema Banyai."Naamini uwepo wake utaimarisha zaidi safu ya ulinzi ya timu yangu pia kuongeza imani kwa wachezaji wengine uwepo wake," aliongeza."Tumba ni mchezaji ambaye ana uzoefu mkubwa na ligi kuu ukizingatia aliwahi kuichezea Azam siku za nyuma," alisisitiza.

Kivutio kikubwa kwenye mchezo huo kitakuwa mshambuliaji wa Moro Utd, Gaudence Mwaikimba akisumbuana na mabeki wa Simba, Juma Nyosso. Simba inaongoza ligi ikiwa na pointi 27 baada ya kushuka dimbani mara 12 ikishinda michezo minane, kutoka sare mitatu na kufungwa mmoja dhidi ya mahasimu Yanga. Imefunga magoli 18 na kufungwa matano.

Wakati, Moro United inashika nafasi ya nane kwenye msimamo wa ligi kwa pointi zake 13 ikiwa imecheza mechi 12 ikishinda mitatu, kutoka sare minne na kupoteza mitano. Imefunga mabao 15 na kufungwa 20.

SHIRIKA LA NDEGE TANZANIA(ATCL) LAFUFUKA SAFARI ZAANZA LEO










Ndege ya shirika la ndege TANZANIA (ATCL)

SHIRIKA la Ndege Tanzania (ATCL), leo linatarajia kuanza safari zake mikoa ya Tabora na Kigoma.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa ATCL, Paul Chizi, alisema ndege hiyo itakuwa ikienda moja kwa moja kwenye mikoa hiyo na safari hizo zitakuwa za kila siku.

“Matayarisho yote yamekamilika na ndege tunatarajia itaanza safari zake kama kawaida kuanzia kesho (leo) Novemba Mosi... tunaomba Watanzania watoe ushirikiano kwa shirika lao kwa kuchagua kusafiri na ATCL, maana ni usafiri wa moja kwa moja wa uhakika na salama,” alisema Chizi.

Chizi alisema Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA), tayari imelipatia shirika cheti cha kuruka kiitwacho Air Operators Certificate (AOC) baada ya kuridhishwa jinsi lilivyotekeleza masharti yake.

Hivi karibuni shirika hilo lilizindua mpango wa biashara (Business Plan) ambao unaeleza jinsi lilivyojizatiti kuhakikisha linamudu ushindani wa usafiri wa anga kipindi cha miaka mitano ijayo.

Mpango huo ulizinduliwa na Naibu Waziri wa Uchukuzi, Dk Athumani Mfutakamba, ambaye alisifu hatua ya shirika hilo kwa mpango huo endelevu, kupata AOC na kulitakia mafanikio mema.

“Nawapongeza kwa kupata cheti cha kuruka, hii ni fursa kubwa kwa Watanzania kuanza kupata huduma za uhakika za shirika lao, naamini mambo yatakwenda vizuri nawatakia mafanikio mema katika mipango yenu mipya,” alisema Dk Mfutakamba.

Serikali katika mwaka wa fedha uliopita ilitenga Sh16.7 bilioni kwa ajili ya kuliwezesha shirika hilo na imeahidi kuendelea kulipa mishahara ya wafanyakazi wa ATCL.

Hata hivyo, katika hali ya kusikitisha wakati shirika linaanza safari zake tena, hakuna hata senti kati ya fedha hizo iliyowekwa kwenye akaunti za ATCL.