Monday, October 24, 2011

FERGUSON AMWAGA CHOZI KATIKA KIPIGO CHA 6-1


Kocha wa Man U, Sir Alex Ferguson alishindwa kuvumilia kipigo cha bao 6 kutoka kwa Man City na kujikuta akilimwaga chozi hadharani...inaumaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa

MAN CITY YAISAMBARATISHA MAN UNITED 6-1 OLD TRAFFORD, "MKORA"BALOTELLI ATUPIA 2 AGUERO 3. ARSENAL YAIADHIBU STOKE VAN PERSIE ATUPIA 2

Balotelli
Balotelli

Kinyume na matarajio ya Wengi, Man United walishindwa kabisa kuhimili vishindo vya majirani zao na mahasimu wao wa jadi. Hadi mapumziko City walikuwa wakiongoza kwa goli moja lililofungwa na Mario Balotelli.

Balotelli akishangilia na ujumbe WHY ALWAYS ME?

Man United walicheza karibu kipindi chote cha pili wakiwa na mchezaji mmoja pungufu baada ya beki Jonny Evans kupewa kadi nyekundu kwa kumzuia Balotelli kwenda kumuona kipa wa United David De Gea.

Video ya matukio na magoli yote Man C vs Man U

Baada ya kutolewa kwa Evans, karamu ya magoli ilianza kwa City. Balotelli aliongeza bao la pili katika dakika ya 60. Sergio Aguero akafunga bao la tatu katika dakika ya 69. Edin Dzeko baada ya kuingia kama mchezaji wa akiba alifunga bao la nne katika dakika ya 90, David Silva bao la tano na Dzeko tena kupiga msumari wa mwisho katika filimbi ya mwisho ya mchezo.

Bao pekee la kufutia machozi la United lilifungwa na Darren Fletcher katika dakika ya 81.

Matokeo haya yanaipa City pointi tatu ambazo zinaifanya kuendelea kuongoza kwa pointi tano zaidi ya United.

Katika michezo mingine, Arsenal iliizaba Stoke City 3-1. Gervino aliandika bao la kwanza katika dakika ya 27, ingawa bao hilo lilisawazishwa na Peter Crouch. Hata hivyo Robin Van Persie ambaye alianza bechi katikika mchezo huo aliingia na kufunga mabao mawili.

Video ya magoli Arsenal vs Stoke City
Everton nayo ikicheza ugenini ilipata ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Fulham. Mabao ya Everton yakifungwa na Royston Drenthe, Luis Saha na Jack Rodwell. Bao la Fulham lilifungwa na Bryan Ruiz.

SIMBA YANGA ZAWABANGUA MAAFANDE KUKUTANA USO KWA MACHO JUMAMOSI 29 Oktoba 2011

SIMBA, juzi walizidi kujiimarisha kileleni mwa Ligi Kuu Bara baada ya kuilaza Ruvu Shooting mabao 2-0, katika mechi iliyopigwa kwenye Uwanja wa Azam Chamazi, Dar es Salaam. Kwa ushindi huo, Simba imefikisha pointi 24 na kuzidi kukalia kiti cha ligi hiyo, huku ikiwa imecheza mechi 10 na kuiacha JKT Oljoro ikiwa ya pili kwa kujikusanyia pointi 19.

Ruvu Shooting walikuwa wa kwanza kulifikia lango la Simba, dakika ya sita, Abdallah Juma, alishindwa kuitumia vizuri nafasi aliyoipata kwa kupiga mpira nje ya lango.

Dakika tano baadaye, Kassim Linde, alishindwa kuitumia vizuri nafasi aliyopata baada ya kupiga shuti lililotoka nje.

Simba walijibu mashambulizi, dakika ya 16, Emmanuel Okwi, alipiga shuti kali lililookolewa na mabeki wa Ruvu Shooting.

Mshambuliaji Uhuru Seleman, dakika ya 25, alipiga shuti kali lililogongwa mwamba wa goli na kuokolewa na mabeki Shooting.

Hassan Dilunga wa Ruvu Shooting, alipata nafasi nzuri ya kufunga dakika ya 42, lakini mpira aliopiga ulitNa Speciroza Joseph

SIMBA, jana walizidi kujiimarisha kileleni mwa Ligi Kuu Bara baada ya kuilaza Ruvu Shooting mabao 2-0, katika mechi iliyopigwa kwenye Uwanja wa Azam Chamazi, Dar es Salaam.

Kwa ushindi huo, Simba imefikisha pointi 24 na kuzidi kukalia kiti cha ligi hiyo, huku ikiwa imecheza mechi 10 na kuiacha JKT Oljoro ikiwa ya pili kwa kujikusanyia pointi 19.

Ruvu Shooting walikuwa wa kwanza kulifikia lango la Simba, dakika ya sita, Abdallah Juma, alishindwa kuitumia vizuri nafasi aliyoipata kwa kupiga mpira nje ya lango.

Dakika tano baadaye, Kassim Linde, alishindwa kuitumia vizuri nafasi aliyopata baada ya kupiga shuti lililotoka nje.

Simba walijibu mashambulizi, dakika ya 16, Emmanuel Okwi, alipiga shuti kali lililookolewa na mabeki wa Ruvu Shooting.

Mshambuliaji Uhuru Seleman, dakika ya 25, alipiga shuti kali lililogongwa mwamba wa goli na kuokolewa na mabeki Shooting.

Hassan Dilunga wa Ruvu Shooting, alipata nafasi nzuri ya kufunga dakika ya 42, lakini mpira aliopiga ulitoka nje ya lango.

Simba, ambao walipata nafasi sita za mpira wa adhabu, lakini walishindwa kuzitumia nafasi hizo.

Dakika ya 47, Okwi, aliwainua mashabiki wa Simba, baada ya kuifungia timu yake bao akitumia vizuri mpira ulioanza kwa Haruna Moshi 'Boban' aliyempasia Jerry Santo, kabla ya mfungaji wa bao hilo kuukwamisha wavuni.

Boban aliyeingia kuchukua nafasi ya Uhuru Seleman, aliifungia bao la pili Simba, dakika ya 54, kwa shuti la mbali lililomshinda kudaki kipa wa Ruvu Shooting, Benjamin Haule.

Bao hilo linakuwa na pili kwa wachezaji wazawa, baada ya Kapombe kufunga katika mechi dhidi ya African Lyon wiki iliyopita. Mabao 12 ya Simba, yamefungwa na wachezaji kutoka nje ya nchi.

Kufungwa kwa bao hilo, kuliwazindua Shooting ambao walikuwa wakisaka mabao ya kusawazisha, hata hivyo walikutana na ngome imara iliyokuwa ikiongozwa na Juma Nyosso na Obadia Mungusa.

Simba: Juma Kaseja, Nassoro Masoud 'Cholo', Juma Jabu, Juma Nyosso, Obadia Mungusa, Patrick Mafisango/Shomari Kapombe, Jerry Santo, Ulimboka Mwakingwe, Emmanuel Okwi, Felix Sunzu, Uhuru Seleman/Haruna Moshi 'Boban'.

Ruvu Shooting: Benjamin Haule, Michael Pius, Paul Ngalema, George Michael, Shaban Suzan, Iddi Nyambiso, Ayoub Kitala, Hassan Dilunga, Abdallah Juma/Seif Abdallah, Kassim Linde/ Juma Mdindi, Raphael Keyala/Abdallah Abdulrahman.
oka nje ya lango.

Simba, ambao walipata nafasi sita za mpira wa adhabu, lakini walishindwa kuzitumia nafasi hizo.

Dakika ya 47, Okwi, aliwainua mashabiki wa Simba, baada ya kuifungia timu yake bao akitumia vizuri mpira ulioanza kwa Haruna Moshi 'Boban' aliyempasia Jerry Santo, kabla ya mfungaji wa bao hilo kuukwamisha wavuni.

Boban aliyeingia kuchukua nafasi ya Uhuru Seleman, aliifungia bao la pili Simba, dakika ya 54, kwa shuti la mbali lililomshinda kudaki kipa wa Ruvu Shooting, Benjamin Haule.

Bao hilo linakuwa na pili kwa wachezaji wazawa, baada ya Kapombe kufunga katika mechi dhidi ya African Lyon wiki iliyopita. Mabao 12 ya Simba, yamefungwa na wachezaji kutoka nje ya nchi.

Kufungwa kwa bao hilo, kuliwazindua Shooting ambao walikuwa wakisaka mabao ya kusawazisha, hata hivyo walikutana na ngome imara iliyokuwa ikiongozwa na Juma Nyosso na Obadia Mungusa.

Simba: Juma Kaseja, Nassoro Masoud 'Cholo', Juma Jabu, Juma Nyosso, Obadia Mungusa, Patrick Mafisango/Shomari Kapombe, Jerry Santo, Ulimboka Mwakingwe, Emmanuel Okwi, Felix Sunzu, Uhuru Seleman/Haruna Moshi 'Boban'.

Ruvu Shooting: Benjamin Haule, Michael Pius, Paul Ngalema, George Michael, Shaban Suzan, Iddi Nyambiso, Ayoub Kitala, Hassan Dilunga, Abdallah Juma/Seif Abdallah, Kassim Linde/ Juma Mdindi, Raphael Keyala/Abdallah Abdulrahman.


YANGA YAISAMBARATISHA JKT OLJORO
Wakati huohuo jana Yanga ya Dar es salaam wameiadhibu Timu ya maafande wa JKT Oljoro kwa bao 1-0 katika uwanja wa Chamanzi nje kidogo ya jiji la Dar es salaam.

Kazi nzuri ya mshambuliaji wa kimataifa Haruna Nyonzima akiwatoka akiwazidi ujanja mabeki wa Oljoro na kutoa pande maridadi kabisa lililomkuta Hamis Kiiza akiwa katika nafasi nzuri ya kushinda nae bila ajizi akaachia kombora kali lilioenda mojo kwa moja kimiani na kuihakikishia timu yake ya Yanga ushindi wa goli 1-0 katika mechi hiyo.

JOKATE MWEGELO APEWA SHAVU SASA NI MTANGAZAJI CHANNEL O
















Jokate kushoto akiwa na watangazaji wenzake wapya wa Channel O.

DStv’s Channel O Africa imemteua mwigizaji na mwanamitindo Jokate Mwegelo kuwa mmoja wa watangazaji wake wapya sita.
Kituo cha televisheni cha Channel O kilifanya usaili nchi mbalimbali na Tanzania ni Jokate aliyefanikiwa kuibuka kidedea.
Washindi wengine wanatoka katika nchi za Nigeria, Uganda, Kenya, Ghana na Afrika kusini.

Kuanzia sasa utakuwa ukimuona Jokate katika mitaa mbalimbali akiwa na kamera na mic za channel O kwa kuwa hiyo ndiyo ajira yake mpya jijini. “Ukikaa karibu na Jokate, umekaa karibu na Channel O”.

Vigezo vilivyotumika kumpata mwakilishi huyo nchini ni kujua vizuri historia ya muziki wa nyumbani na vitu vingine mbalimbali kwani ndivyo atakavyotakiwa kuripoti.