Tuesday, September 20, 2011

Mourinho aigawa zawadi ya kocha bora wa Dunia kwenye mfuko wa Bobby Robson


Mourinho akimkabidhi zawadi hiyo

Bosi wa Real Madrid Jose Mourinho ametoa zawadi yake ya kujivunia ya kocha bora wa mwaka ili ipigwe mnada na fedha ziingizwe katika mfuko wa Sir Bobby Robson unaopambana na kansa.
Mourinho amefanya kazi na Bobby akiwa Sporting Lisbon,Porto na Barcelona na kujifunza kuwa meneja bora wa timu.
Mourinho atatoa tuzo hiyo ya kocha bora wa dunia aliyoipata akiwa na klabu ya Inter Milan 2010 na itapiogwa mnada katika mtandao mwezi ujao na yule atakae dau kubwa ndio atainyakua tuzo hiyo na fedha kuelekezwa kwenye mfuko wa Sir Bobby Robson.
Mnada huo utafanyika kuanzia tarehe 8-23 sambamba na mchezo wa hisani wa soka katika uwanja wa Burry St Edmunds,Suffolk.