Monday, August 29, 2011

VIDEO YA MAGOLI YOTE NANE NA MATUKIO MUHIMU MAN UNITED VS ARSENAL

Man United walipoiadhiri Arsenal 8-2

Real Madrid Yaiadhibu Zaragoza 6-0 Ronaldo apiga "hat trick"

Real madrid imeifumua Real Zaragoza nyumbani kwao kwa jumla ya mabao 6-0 magoli yakifungwa na Alonso,Kaka,Marcello na Ronaldo akitia tatu takatifu.

Alonso kifunga goli la 3


Ronaldo akifunga goli la nne


Kaka akifunga goli la 5


Ronaldo akifunga goli la sita na la tatu kwake katika mechi hiyo.


Marcelo akifunga goli la 2


Magoli yote sita

WENGER AFUNGUKA PAMOJA NA KIPIGO CHA AIBU SIBANDUKI NG'O


Ferguson akimpoza Wenger

Kocha wa kitambo wa Timu ya Arsenal Arsene Wenger amesema anahitaji kuongeza wachezaji watatu na akafunguka kuwa hatoki kamwe katika timu hiyo japokuwa amepata pointi moja tu katika michezo mitatu msimu huu. Wenger aliyasema hayo katika mahojiano yake na waandishi wa habari baada ya kupata kipigo kitakatifu kutoka kwa Man United cha 8-2 katika mechi ya ligi kuu Uingereza inayoendelea katika msimu wa 2011-2012.

CHELSEA YAIADHIBU NORWICH CITY 3-0

Juan Mata
Juan Mata

Juan Mata katika mechi yake ya kwanza katika uwanja wa Chelsea wa Stamford Bridge, aliweza kufunga bao lake la kwanza akiichezea timu yake mpya, na kuiwezesha kusonga hadi kuongoza ligi kuu ya Premier, angalau kwa muda mfupi, baada ya kuifunga Norwich magoli 3-1.

Liverpool baadaye ilijipenyeza hadi nafasi ya kwanza, kwa kupata ushindi kama huohuo, ilipocheza katika uwanja wa nyumbani wa Anfield dhidi ya Bolton na kuizaba magoli 3-1.

Hata hivyo, licha ya kupata ushindi, mashabiki wengi wanafikiria kwamba Chelsea haikucheza kama ilivyotazamiwa.

Chelsea walikuwa wa kwanza kupata bao, kupitia mchezaji Jose Bosingwa, lakini Norwich wakasawazisha kupitia mchezaji Grant Holt.

Frank Lampard alitia wavuni mkwaju wa penalti na kuongeza mabao hadi 2-1, baada ya kipa John Ruddy kumwangusha Ramires, akihisi mchezaji huyo wa Chelsea alikuwa anajiandaa kufunga.

Mata aliiandikishia Chelsea ushindi, lakini raha ya ushindi huo kugubikwa na kutojua hali ya Didier Drogba ni vipi, baada ya kujeruhiwa kichwa.

Kipa Ruddy alikuwa anajaribu kuondosha mpira alipompiga ngumi ya uso Drogba.

Katika mechi nyingine, Aston Villa na Wolves walishindwa kufungana, na mechi kwisha 0-0.

Matokeo yalikuwa ni kama hayo pia katika mechi kati ya Swansea na Sunderland.

Everton iliwafunga Blackburn goli 1-0.

Wigan nayo iliwafunga QPR magoli 2-0.

Kuhusiana na Liverpool kuishinda Bolton na kuwa kileleni, meneja Kenny Dalglish ameisifu timu yake ya Liverpool, akisema walionyesha wazi kwamba waling'ara katika uwanja wa Anfield.

Kenny Dalglish
Meneja wa Liverpool amewasifu wachezaji wake kwa kuwa kileleni katika ligi kuu ya Premier

"Ilikuwa ni burudani kutazama walivyocheza," alielezea baadaye, kufuatia mabao kutoka kwa Jordan Henderson, Charlie Adam na Martin Skrtel.

Meneja wa Bolton Owen Coyle alikiri kwamba Liverpool walistahili ushindi wao wa magoli 3-1 lakini akaongezea: "Tulijiharibia wenyewe mwanzo wa kipindi cha pili kwa kuwaruhusu kutufunga magoli mawili zaidi."

Bao la Ivan Klasnic ambalo lilipatikana katika dakika za mwishomwisho katika mechi halikuwapa faraja yoyote Bolton.

MAN UNITED YAISULUBU ARSENAL KWA MISUMARI 8-2 MAN CITY YAICHAKAZA HOTSPURS

Wayne Rooney amepachika mabao matatu peke yake wakati Manchester United ikiinyuka Arsenal kwa mabao 8-2.
Young
Young na Rooney



Danny Welbeck ndiye alifungua karamu ya magoli baada ya kuunganisha pasi ya Anderson.

David De Gea aliokoa penati iliyopigwa na Robin Van Persi, na baadaye kidogo Ashely Young kufunga bao la pili.

Rooney aliandika bao la tatu na la nne kwa mikwaju miwili ya adhabu, kabla ya kufunga bao moja kwa mkwaju wa penati.

Nani na Park Ji Sung walifunga nao na Ashley Young kuongeza jingine.

Mabao ya Arsenal yalifungwa na Theo Walcott na Robin Van Persie.

Awali Manchester City waliizaba Tottenham Hotspur kwa mabao 5-1.

Edin Dzeko alifunga mabao manne, na Sergio Aguero akifunga moja. Bao pekee la Spurs lilifungwa na Younis Kaboul.

Kwingineko Newcastle United imeibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Fulham. Leon Best akifunga mabao yote ya Newcastle na goli la Fulham kufungwa na Clint Dempsey.

West Brom walishindwa kuutumia vyema uwanja wao wa nyumbani baada ya kuchapwa bao 1-0 na Stoke City. Goli hilo pekee lilifungwa na beki Ryan Shotton katika dakika ya 89.

Mateka 50,000 wapo chini ya Gaddafi na hawajulikani walipo

Waasi wa Libya wanasema wana wasiwasi na hatma ya maelfu ya wafungwa ambao walikuwa wakishikiliwa na utawala wa Gaddafi.
Waasi wasaka nyumba ya wafuasi wa Gaddafi

Msemaji wa kijeshi wa waasi Kanali Ahmed Omar Bani amesema watu wapatao elfu 50 waliokamatwa miezi ya karibuni hawajulikani walipo.
Waasi wanaamnini kuwa wafungwa hao huenda wanashikiliwa katika maghala ya kijeshi yaliyoko chini ya ardhi, ambayo yametelekezwa.
Vikundi vya kutetea haki za binadamu vina ushahidi kwamba watu wengi wameuawa karibu na magereza, lakini Kanali Bani hajamshutumu yeyote kwa mauaji ya wafungwa hao.
"Idadi ya watu waliokamatwa kwa miezi kadha iliyopita inakadiriwa kuwa kati ya 57,000 na 60,000," amesema katika mkutano wa waandishi wa habari mjini Benghazi."Mpaka sasa, Kati ya wafungwa 10,000 na 11,000 wameachiliwa huru... wengine wako wapi?"
Kanali Bani ameomba kwa yeyote mwenye taarifa kuhusu wafungwa hao kujitokeza, na amesema itakuwa jambo la kutisha iwapo wameuawa.
kuna hofu kuwa maelfu ya wateka wangali wanashikiliwa katika jela lililojengwa chini ya ardhi ambako inasaidikiwa kuwa wamekimbiwa na majeshi ya Kanali Gaddafi wakati waasi walipoingia Tripoli na kuuteka nyara.
Kinachoendelea kwa wakati huu ni pilka pilka za kuwatafuta mateka hao ambao hawajulikano waliko ili waachwe huru.
Al-Megrahi

wakati huo huo viongozi waasi wamesema hawana nia yakumrudisha Abdel Basset al-Megrahi ambaye mwaka 1988 alifungwa jela kwa kulipuwa ndege ya Lockerbie katika anga ya Scotland.
Megrahi aliachiliwa mapema kutika jela miaka miwili iliyopita baada ya madaktari kudai anakaribia kufariki kwani ana miezi michache tu ya kuishi . kuachiliwa kwake kulipingwa na wengi.
Lakini hivi majuzi kumekuwa na shinikozo za kumtaka Megrahi arudishwe uingereza au akafunguliwe amshitaka upya nchini Marekani.
Na shirika la harabi la CNN limemkuta bwana huyo katika jumba la kifahari viungani mwa mji wa Tripoli lakini akiwa mahututi chini ya uangalizi wa familia yake.