Friday, August 19, 2011

MNARA UNAOTAJWA KUWA MREFU KULIKO YOTE DUNIANI WAANZA KUJENGWA

Ujenzi wa mnara unaotarajiwa kuwa mrefu kuliko yote ambayo imepata kutokea duniani umeanza, Unatarajiwa kupewa jina la KINGDOM TOWER. Mnara huo unajengwa nchini Saudi Arabia na unatarajiwa kuwa na urefu wa zaidi ya futi 3000 na unatarajiwa kugharimu zaidi ya dola bilioni moja.
Mnara utakapokamilika muonekano uwapo mnarani utakuwa wa ajabu sana, ambapo ni zaidi ya 2/3 ya maili moja, utakuwa na maeneo ya biashara,maduka na sehemu za starehe.
Zifuatazo ni picha zitakazotokana na mnara huo pindi utakapokamilika.


 Tallest-tower
Manjonjo ya mnara huo sehemu ya juu na jinsi utakavyoonekan kwa mbele ukiwa Bahari ya Hindi.

Kingdom Tower
Taswira halisi ya mnara huo itakavyokuwa.


Tall Tower
Mandhari ya Kingdom Tower yatakavyokuwa sehemu ya chini.

JUKWAA LAANGUKA WAKATI WA TAMASHA LA MUZIKI NA KUUA

Nchini Ubelgiji jukwaa limeanguka na kuua watu kadhaa, Jukwaa hilo lilianguka katka tamasha la muziki linalojulikana kama Pukkelpop Music Festival jijini Hasselt, watu wanne wameripotiwa mapema kufariki dunia katika tukio hilo.

Belgium-Pukkelpop
Watu wakiwa wamepigwa na butwaa katika tukio hilo.

Msanii Cullen Omori amekaririwa mapema leo hii akisema "Ndio kwanza tulikuwa tumemaliza kuimba wimbo wetu wa kwanza katika nyimbo zetu hapa Pukkelpop, ndipo jukwaa na hema vikaanza kutingishika na tukafikiri labda ni kimbunga tu kinapita, ndipo nikaamrisha tuendelee na wimbo wa pili ndipo meneja wa msafara alisikika akipiga yowe kuwa tuteremke kutoka jukwaani, mara ghafla upande mmoja ukaanguka futi moja kwenda chini, tukafikiri kuwa ni jukwaa tu ndio limeanguka na sio hema ghafla vilio na kelele vilitosha kutueleza kilichotokea, lakini mpaka wanauja waokoaji na kututaarifu kuwa kuna watu waliopoteza maisha wapatao wanne na kadhaa wamejeruhiwa, huruma na mawazo yetu yakawa kwa wale waliowapoteza wapendwa wao katika janga hili."

Tazama jinsi ilivyokuwa

FAHAMU WATU MAARUFU WAMESEMA NINI WIKI HII

 photo | Jennifer Hudson
Jennifer Hudson "Najivunia kupungua uzito kuliko tuzo yangu ya Oscar"


 photo | Emma Stone, Jimmy Kimmel
Emma Stone amefunguka na kusema "It's a fake farm, but it doesn't feel fake, Jimmy. I was leaving dinners to harvest." Na kwa maneno hayo anasema ndio maana alijitoa Facebook.




 photo | Amber Heard
Amber Heard amefunguka na kusema "To say I came out implies that I was once in. Let me be straight about that – no pun intended [laughs] – I never came out from anywhere." Nyota huyo wa klabu ya Play Boy ameyasema hayo huku akitanabaisha kuwa huwa hafichi mahusiano yake lakini anapenda kuyafanya maisha yake binafsi kuwa ya siri.




 photo | Nicole Polizzi
Nae Nicole "snooki" Pollizi amefunguka na kushare na mashabiki wake mambo yake ya faragha kwa kusema "When I'm really excited about something, I poop."




 photo | Jimmy Kimmel, Kate Gosselin
Kate nae anafunguka hivi kuhusiana na suala la watoto "[Kate said] she will now devote more time to motivational speaking. Why not? She's already motivated millions of people to not have kids.





Caroline Gonzalez msichana mwenye umri wa nyundo 11 anafunguka na kusema "I like his music and I like him. And I thought, why not have a street in my hometown named after my favorite singer?"  Aliyasema hayo wakati akiupatia mtaa jina katika kitongoji cha Forney jijini Texas, alipochaguliwa kuwa meya wa siku moja.




 photo | Kim Kardashian, Tyra Banks
Tyra Banks nae anafunguka kuhusiana na harusi ya Kim Kardashian inayotarajiwa hivi karibuni "Nothing! A kiss and a congratulations."




BOB JUNIOR SIO SHOGA NI SANAA

Hivi karibuni katika vyombo vya habari vingi kumekuwa na habari ambayo imebamba vilivyo, nayo ni kumhusu mtayarishaji na msanii wa muziki wa kizazi kipya Bongo flava,huyu si mwingine ni Rais wa Masharobaro Raheem Nanji a.k.a Bob Junior, ikisemekana kwamba kukatika kwake viuno katika kazi yake ya muziki kuna uhuziano na yeye kuwa shoga, Nimeshindwa kujizuia nikiwa shabiki wake namba moja na shabiki wa sanaa ya muziki huu wa bongo flava kusikia mtu akisingiziwa vitu ambavyo havipo kwasababu ya sanaa.

Raheem Nanji a.k.a Bob Junior

Huu ni ushamba kumtafsiri mtu tofauti na vile alivyo, kukata viuno ni kazi ya sanaa kwani wacheza show za muziki huwa wanafanya nini? hata hivyo wasanii wangapi duniani wanakata viuno? mbona hata Mr Nice enzi hizo alikuwa viuno kwa kwenda mbele,je ni shoga? H Baba nae hivyohivyo,je ni shoga? Fally Ipupa nae,je ni SHOGA? Acheni kufuatilia maisha ya mtu kama mnapenda muziki pendeni muziki kama hampendi kazi zake mpotezeeni acheni kumfuatafuata katika maisha binafsi. Hata kama ni shoga yanawahusu? kuweni basi na nyinyi mashoga kama mnamuonea wivu.

Elton John na wengine maarufu ni mashoga na wapo juu ile mbaya mbona hamsemi? acheni hizo kwanza nafikiri hamjui nini maana ya sanaa au nini maana ya msanii ndio maaana mnakurupuka na kumpakazia Bob Junior. Bob Junior kama unisoma hii mzee nakushauri makamuzi ya viuno kwa kwenda mbele asiependa kazi zako na akupotezee sio lazima awe fan wako, hiyo ni sanaa na lazima msanii aheshimiwe kulingana na hisia na mawazo yake, Bob Junior be more concerned with your character than reputation, because a character is what really you are and reputation is what people think you are...wapotezeeeeeee.
Labda kwa faida ya wasiojua nini maana ya msanii au sanaa,
Kwanza Sanaa ni dhima ya upangaji wa dhana kulingana na hisia na mawazo ya msanii,
Pili Msanii sasa ndio mtu anaepanga dhana kulingana na hisia na mawazo yake.

Sasa basi Bob Junior anahaki ya kufanya kazi vile hisia na mawazo yake yanavyomtuma ili kukamilisha kazi yake ya usanii na kazi hiyo isitafsiriwe kuwa ni ushoga kwani sanaa itabaki kuwa sanaa na ushoga utabaki kuwa ushoga na ndio maana nikasema Bob Junior ameona staili ya viuno ndio inaendana na hisia zake,basi tumheshimu kama kuna mengine hayahusu katika kazi zake, au mmepandikizwa na wasanii wanaomuonea wivu kwa kazi zake naweza kuwaelewa lakini sio kiivyo.

SONGI LA LEO

Linex na wimbo wa moyo wa subira