Thursday, July 28, 2011

TOLEO JIPYA LA TRENI JAPAN

Hakika Japan wapo mbali katika teknolojia, wakati sisi huku bado tunapanda "vyuma chakavu" wenzetu Japan wanakula bata..hakika toleo hili ni zaidi ya ndege.



sehemu ya abiria

maeneo ya kuelekea chooni



Abiria wakijiandaa kukwea mchuma

Treni ikikatiza mitaa

Treni ikiingia stesheni

sehemu ya dereva wa treni

WANIGERIA WAZICHAPA NDANI YA JUMBA LA BIG BROTHER AFRICA

Asubuhi ya leo Karen alimshambulia Vina kwa maneno akimshutumu na kumpasha kwa kujipendekeza kwa Lomwe wakati hamtaki hali iliyozua tafaruku kati ya mabinti hao ndani ya jumba la Big Brother africa, Karen na Vina wote wanatoka Nigeria.

Karen (kushoto) na Vina (kulia)
Awali mabinti hao walishutumiana katika vitu fulanifulani na kuanza kushikana nguo hali iliyomfanya Hanni aingilie kati ili kunusuru amani baina ya mabinti hao wawili, "mmoja akiwa moto, lazima mmoja awe maji" alisikika Hanni akiwasihi mabinti hao waache ugomvi, Kitendo cha Hanni kumsihi Vina aachane na Karen na amzoee kwani ndivyo alivyo kilionekana kumjaza ghadhabu zaidi Karen, ambapo ugomvi huo ulianza 26 julai, siku ambayo ilikuwa ni birthday ya Vina, siku hiyo Vina alibainisha kuwa Karen utani wake umezidi mipaka na sasa sio utani tena bali ni kusambaza uongo. Zikiwa zimebaki siku mbili.je wanigeria hao wataweza kushinda?

SHEREHE ZA MWAKA MMOJA KUELEKEA OLIMPIKI 2012

Sherehe zinafanyika jijini London kuadhimisha mwaka mmoja kamili kabla ya kuanza michezo ya Olimpiki ya mwaka 2012.

Uwanja utakaotumika kwa olimpiki UK 2012
Kituo cha kuogelea katika Olympic Park , Stratford kitazinduliwa na anaetarajiwa kushinda medali ya Olimpiki Tom Daley akiwa mchezaji wa kwanza kupiga mbizi.
Rais wa Kamati ya Kimataifa ya Olympiki (IOC) Jacques Rogge atakua katika uwanja wa Trafalgar Square ambako mifano ya medali zitakazokua zikitolewa katika michezo hiyo zitazinduliwa.
Mwenyekiti wa Kamarti ya matayarisho ya Olimpiki 2012 Lord Coe amesema mipango yote imekwenda kama ilivyopangwa.
Amesema hii ni siku kubwa kwa kamati ya matayarisho akiongeza kuwa wamepokea maombi millioni 23 ya tiketi kutoka watu milioni mbili na kwamba watu laki mbili na elfu 50 wamejitolea kutumika wakati wa michezo hii.
Katika sherehe za Trafalgar Square, usiku Bwana Rogge na Meya wa jiji la London, Boris Johnson wataialika dunia kuja London kusherehekea michezo hii majira ya kiangazi mwakani.
Bendi ya muziki wa Pop, The Feeling, kwaya za nyimbo za dini na na DJ wa Radio 1 DJ Kissey Sell Out ni miongoni mwa watakaotumbuiza.

DVD YA UMEME OUT SASA SAMAKI WENYE SUMU SIJUI IPI ITAFUATA

SERIKALI HII KIBOKO..KABLA HATUJAMALIZA KUANGALIA DVD YA UMEME TAYARI WAMEIKATISHA NA HATUJAJUA MWISHO WAKE NI NINI..STERLING NGELEJE ATAKUFA AU? HAYA WAMETUWEKEA DVD YA SAMAKI WA SUMU KUTOKA JAPAN..LAKINI PICHA HII NAYO INAONEKANA NI KALI SANA INGAWAJE WASIWASI WANGU ULEULE KUWA PICHA LIKINOGA NA WAKATI WATU TUMESHAAGIZA POP CORN NA TUMEKAA ZETU SAWA SAWA KATIKA SOFA ILI TUICHEKI KWA UZURI WATATUBADILISHIA NYINGINE, SIPENDI MCHEZO WA KUTOKUMALIZIA MOVIE ILA SINA JINSI NA SISI WENYEWE TUNAYATAKA INATAKIWA TUKOMAE MPAKA MOVIE MOJA IKIISHA WATUWEKEE NYINGINE LAKINI TUNAWAACHIA MOVIE ZIKIKOLEA WAO NDIO WANATOA.


ILA NIWAPONGEZE HIZI DVD WANAPOZIPATA MAANA KILA INAYOKUJA NI KALI KUPITA ILIYOTOLEWA,KWA HILI VIONGOZI WA TANZANIA NAWAPA 100% WAMEFUZU MAFUNZO YA KUSIMAMIA MABANDA YA VIDEO.
LAKINI HUWA NAJIULIZA UTAALAMU HUU LAZIMA KUNA MTU NYUMA YA PAZIA ANAEWAWEZESHA KUWA MAHODARI KIASI HIKI,JE NI NANI?..BILA SHAKA HAKUNA ASIEMJUA NI YULE Dk WETU..NAE NAMSIFU SANA WAKATI SISI TUNAKETI KUCHEKI MOVIE TULIYOWEKEWA YEYE HUISHIA KUTABASAMU TU BILA KUJALI HIYO MOVIE TULIYOWEKEWA KUWA INA MADHARA.

MADHARA HAYO NI PAMOJA NA KUTUUMIZA MACHO, INATUFANYA TUSHINDWE HATA KUONA VIZURI HALI INAYOPELEKEA TUNASHINDWA KUFAHAMU MAMBO TUNABAKI KUWA MAMBUMBUMBU TU TUKIACHA VITU VYA HOVYOHOVYO VIKIFANYIKA KATIKA ARDHI YETU.

PILI, HIZI MOVIE ZINAFANYA TUNATUMIA MUDA MWINGI KUZIANGALIA MPAKA TUNASHINDWA KUFANYA KAZI NA KUJIPATIA KIPATO NA KWA HALI HUU TUNADUMISHA UMASKINI KWETU NA KWA TAIFA KWA UJUMLA.

VILEVILE HIZI MOVIE ZINATUKOMAZA NA MATATIZO NA MBAYA ZAIDI SASA ZINAELEKEA KUTUFUMBUA MACHO KWA KUONA KILE KINACHOFANYIKA KATIKA MOVIE HIZI SI SAHIHI.

HAPA SASA MIMI NDIPO NINAPOOGOPA NA NINAKUOMBA Dk,sijui ni Dk wa NINI MSINIULIZE HATA MIFUGO SI NI Dk? WA KIENYEJI NAE SI NI Dk?..tafadhali TUNAELEKEA PABAYA NA HIZI MOVIE, KWA HIVI SASA TAYARI WALE WATAZAMAJI WAMESHAANZA KUZICHAMBUA NA KUJUA KILICHOMO KATIKA HILI BANDA LA VIDEO, MBAYA ZAIDI WAMESHAGUNDUA KWANINI MOVIE HAZIMALIZIWI, WAMEGUNDUA HAZIMALIZIWI KWASABABU MOVIE ZOTE HIZI WALE MA-STERLING WANATAKIWA WAFE NA KWA KUWA ZINATOLEWA MAPEMA NAKUWEKWA ZINGINE NDIO MAANA HAWAFI WANAPETA TU WAKATI WAMESHAFANYA UHALIFU MKUBWA KATIKA TAIFA.
USHAURI WANGU KWAKO Dk..TAFADHALI WAAMURU WALE WABADILISHAJI MIKANDA(DVD) PINDI DVD INAPOWEKWA HALAHALA MPAKA TUONE MWISHO WA PICHA NA TUHAKIKISHE STERLING AMEKUFA NDIO TUANGALIE MOVIE NYINGINE,NA KAMA HAJAFA BASI AWE SHUPAVU SANA KUWAPIGA MAADUI WOTE NA ABAKI PEKE YAKE.
PILI, HAKIKISHA MOVIE HAZIRUDIWI NA KABLA SIJAENDELEA KUKUPA USHAURI NINA SWALI..HIVI UNAFIKIRI HAWA MA-STERLING WAKIFA NA KAMA HAWAJAFA UKIWAUA UTAKOSA WENGINE?...UTAKAPO NIJIBU NDIO NITAENDELEA KUKUPA USHAURI ZAIDI NA HII NI KWA FAID YA TAIFA...SALAMU ZANGU KWAKO Dk.