Wednesday, July 27, 2011

BATISTA ATIMULIWA ARGENTINA

Sergio Batista amekubali kuacha ukocha wa timu ya taifa ya Argentina baada ya nchi hiyo kutolewa hatua ya robo fainali ya kuwania kombe la Copa America.

Sergio Batista
Wenyeji Argentina walitolewa na mabingwa Uruguay kwa mikwaju ya penalti.
Batista, mwenye umri wa miaka 48, amekuwa akiifundisha Argentina kwa mwaka mmoja sasa, awali akiwa kocha wa muda, baada ya Diego Maradona kutimuliwa kufuatia kutolewa katika Kombe la Dunia mwaka 2010.
Msemaji wa Chama cha Soka cha Argentina (AFA) amesema Batista hajatimuliwa, lakini imeamuliwa "kutengua" mkataba wake.
Argentina, ambayo mara ya mwisho kunyakua kombe muhimu ilikuwa mwaka 1993 waliposhinda mashindano ya Copa America, wamefuta mechi ya kirafiki dhidhi ya Romania mjini Bucharest iliyopangwa kuchezwa tarehe 10 mwezi wa Agosti.
"Makocha wa Argentina kwa viwango vyote wanafanyiwa tathmini na tume ta makocha wa taifa," aliongeza Bialo.
"Hakuna muda maalum uliowekwa, hakuna sababu ya kuharakisha kumchagua kocha mpya, kwa hiyo kuna mchakato wa kuwasoma na kuwafikiria makocha."

BECKHAM AMTETEA BALOTELLI

David Beckham amemtetea Mario Balotelli kutokana na utata uliojitokea wakati akiwa karibu na lango alipoupiga mpira kwa kisigino badala ya kufunga, hali iliyomsabababishia atolewa nje na meneja wake wakati Manchester City ilipopambana na LA Galaxy.

Balotelli

Meneja wa Manchester City Roberto Mancini alihoji umahiri wa mchezaji huyo baada ya makusudi kukataa kufunga bao la wazi.
"Niliangalia tena, kutokana na tabia yake, naamini alidhani alikuwa ameotea," alisema Beckham, huku akimshauri Balotelli aendelee kufunga katika mechi zijazo.
"Mario amekuwa mchezaji hodari kwa miaka michache iliyopita na bado ni kijana mdogo sana."
Nahodha huyo wa zamani wa England, ambaye aliwahi kuichezea Manchester United ambao ni mahasimu wakubwa wa Manchester City, ameongeza: "Ataendelea kurjirekebisha, nina hakika.
"Lakini iwapo unadhani umeotea au la, hiyo haina maana. Kuna vijana wengi wadogo wanaziangalia hizi timu na wachezaji nyota waliokuja hapa.. Ni lazima uoneshe umahiri wako an ufunge bao."
Mancini, ambaye alizozana na Balotelli wakati akitoka uwanjani baada ya dakika 31, amesisitiza mshambuliaji huyo alipokuwa Inter Milan na yeye akiwa meneja wake alijua hakuwa ameotea.
"Katika soka kila wakati unatakiwa kuonesha umahiri, kila wakati unakuwa makini na kwa wakati ule hakuwa makini na hakuonesha umahiri wake," alisema.