Tuesday, July 26, 2011

RATIBA LEAGUE 1 (UFARANSA) AGOSTI 6-14


Saturday 6th August
20:00AC Ajaccio vs Toulouse
20:00AS Nancy vs Lille
20:00Brest vs Evian TG
20:00Caen vs Valenciennes
20:00Marseille vs Sochaux
20:00Montpellier vs Auxerre
20:00Nice vs Lyon
20:00PSG vs Lorient
Sunday 7th August
16:00Dijon vs Rennes
20:00Bordeaux vs St Etienne
Saturday 13th August
18:00Lorient vs Bordeaux
18:00Lyon vs AC Ajaccio
18:00Rennes vs PSG
18:00Sochaux vs Caen
18:00St Etienne vs AS Nancy
18:00Toulouse vs Dijon
20:00Valenciennes vs Brest
Sunday 14th August
16:00Auxerre vs Marseille
16:00Evian TG vs Nice
20:00Lille vs Montpellier

RATIBA BUNDESLIGA AGOSTI 5-AGOSTI 20


Friday 5th August
19:30Borussia Dortmund vs Hamburg
Saturday 6th August
14:30Augsburg vs SC Freiburg
14:30Cologne vs Wolfsburg
14:30Hannover 96 vs TSG Hoffenheim
14:30VfB Stuttgart vs Schalke 04
14:30Werder Bremen vs FC Kaiserslautern
17:30Hertha Berlin vs Nurnberg
Sunday 7th August
14:30Mainz vs Bayer Leverkusen
16:30Bayern Munich vs Borussia M'gladbach
Saturday 13th August
14:30Hamburg vs Hertha Berlin
14:30Nurnberg vs Hannover 96
14:30SC Freiburg vs Mainz
14:30Schalke 04 vs Cologne
14:30TSG Hoffenheim vs Borussia Dortmund
14:30Wolfsburg vs Bayern Munich
17:30Borussia M'gladbach vs VfB Stuttgart
Sunday 14th August
14:30FC Kaiserslautern vs Augsburg
16:30Bayer Leverkusen vs Werder Bremen
Friday 19th August
19:30Borussia M'gladbach vs Wolfsburg
Saturday 20th August
14:30Augsburg vs TSG Hoffenheim

HOFFENHEIM KUIPIKU CELTIC KUMSAJILI MUSONA TOKA KAIZER CHIEFS

Timu ya Hoffeinheim ya Ujerumani ina matumaini makubwa ya kuizidi kete klabu ya Celtic ya Uskotchi katika mbio za kumuwania mshambuliaji mzimbabwe Musona mwenye umri wa miaka 21 anaekipiga Kaizer Chiefs ya kusini mwa afrika.
Musona
Katika ligi ya Afrika ya kusini iliyoisha Musona aliweka rekodi ya kufunga magoli 15 katika mechi 28 alizocheza katika ligi hiyo na kishawishi Celtic kutangaza ofa ya dau la paundi za Uingereza 2.2 milioni ili kumsajili mchezaji huyo. Lakini wajerumani wanaona Musona ndio chaguo sahihi katika kuziba pengo la Mghana Prince Tagoe waliemtoa kwa mkopo kwenda Partizan Belgrade baada ya kutofanya vizuri tangu alipojiunga na timu hiyo mwaka 2009 akiwa amefunga magoli mawili tu katika mechi 19 alizocheza katika ligi hiyo ya Ujerumani maarufu kama "Bundesliga" Ingawaje matumaini ya kumnasa Musona yanaweza kufifia kutokana na ukweli kuwa timu ya Hoffeinheim imetangaza dau dogo la paundi za Uingereza 1.3 milioni ukilinganisha na dau lililotolewa na Celtic la paundi za uingereza 2.2 milioni.

MAGOLI YA FAINALI COPA AMERICA URUGUAY ILIPOINYANYASA PARAGUAY

Suarez, Forlan waonesha viwango.

MANCINI ANA MATUMAINI YA KUMNASA SERGIO AGUERO

Meneja wa Man City Roberto Mancini amefunguka na kusema kuwa ana matumaini makubwa ya kumnasa Sergio Aguero kutoka Atletico Madrid mwishoni mwa wiki hii. Man C inafungua milango ya maongezi na Atletico Madrid kwa kuwa Srgio amekuwa ni mmoja kati ya wachezaji anaowahitaji katika kikosi chake.
Sergio Aguero
Pamoja na upinzani uliopo kutoka kwa Real Madrid na Juventus ambao nao wanatajwa kumuwania Sergio lakini Mancini ana matumaini ya kushinda kinyang'anyiro hicho mwishoni mwa mwezi huu."Sielewi kwa sasa lakini ninachojua Atletico walikuwa na maongezi na Sergio kabla ya mwisho wa wiki" alisema Mancini.
"Nafikiri kati ya siku nne au tano kabla ya mechi inayofuata,na inaweza kuwa wiki hii tukamaliza mazungumzo"Alioneza Mancini.
"Aguero amecheza Copa America, kama tukikubalina nataka nizungumze nae mwenyewe kwasababu nataka nijue maoni yake(kuhusu kucheza Manchester City)" Alifunguka zaidi kocha huyo wa Manchester City.

ASTON VILLA YAKUBALI KUTOA DAU KUMNYAKA N'ZOGBIA TOKA WIGAN

Charles N'zogbia
Aston Villa imefungua milango ya maongezi na Wigan Athletic juu ya kumsajili Charles N'zogbia mwenye umri wa miaka 25 na imekubali kulipa ada ya uhamisho ya paundi za uingereza 9.5 milioni. Meneja wa Villa Alex Mc Leish ameridhishwa na kiwango cha N'zogbia na timu yake imeamua kufanya mazungumzo rasmi na Wigan ili kumsajili mchezaji huyo. Habari kutoka ndani ya klabu ya Villa zinasema pesa ipo ya usajili baada ya kumuuza Ashley Young kwenda Man United na Stewart Downing kwenda Liverpool zote za uingereza, kabla ya kusaini mkataba mrefu ndani ya Villa N'zogbia anatarajiwa kwanza kufanyiwa vipimo vya afya.

FERGUSON ASEMA AMERIDHIKA NA WACHEZAJI KWA SASA

Kocha wa Manchester United Sir Alex Ferguson anasema hatomsajili mchezaji yoyote hadi pale watakapokabiliana na majirani zao Manchester City katika uwanja wa Wembley.

Sir Alex Ferguson
Tayari ameshamsajili Ashley Young, Phil Jones na mlinda mlango David de Gea.
Kiungo wa Inter Milan Wesley Sneijder amehusishwa na Manchester United.
Lakini Ferguson anasema: "kwa wakati huu,sioni ya kuongeza mchezaji mwengine. Mchezaji ambaye tunamuhitaji hatujamuona kwa sasa."
Aliongeza kuwa: " Tumepoteza wachezaji watano mwaka huu kutokana na wao kuwa na umri wa miaka zaidi ya thelathini".
"Hilo limetusaidia kupata pesa za kuwasajili wachezaji watatu vijana niliowaleta kwenye timu.
"Nimeridhika na wachezaji nilionao kwa sasa."
Kutokana na kustaafu kwa kiungo Paul Scholes,majina kadhaa yametajwa kama yanayofikiriwa kujumuishwa kwenye kikosi cha Manchester United kama vile Sneijder, Samir Nasri wa Arsenal na Luka Modric wa Tottenham.
Hata hivyo Ferguson amekanusha kama anafikiria kumsajili Sneijder, akisema kwamba "hana nia ya kumsajili".