Wednesday, June 8, 2011

WANYAMA NI RAFIKI WAZURI KWA BINADAMU.

Hapa duniani kiumbe ambaye amepewa akili ya kuweza kuufahamu ulimwengu na kuutawala ni Binaadamu, Pamoja na hilo maisha ya Binaadamu yanategemea viumbe wengine waliomzunguka kwa asilimia kubwa,mfano binaadamu wanategemea wanyama kwa kupata chakula mfano,Ng'ombe,mbuzi,nguruwe,kondoo na wengineo wengi. Binaadamu anategemea wanyama wengine kwa kazi za kila siku mfano,Punda kubeba mizigo, Ng'ombe kulimia na hata ubebaji wa mizigo. vilevile Binaadamu anategemea wanyama kwa ulinzi kwa mfano Mbwa.
Lakini baadhi ya wanyama wametokea kuwa adui wakubwa kwa Binaadamu kwa mfano Simba,Chui,Nyoka,na wengineo wengi. Lakini nimegundua kuwa Binaadamu na wanyama wanaogopana kwasababu hawajajuana, lakini pindi Mnyama anapokuwa karibu na akawa na mazoea na Binaadamu basi huwa rafiki mzuri sana wa Binaadamu kwa mfano Simba,Chui,Mbwa,Dubu ,Nyoka na wengineo wengi.angalia picha zifuatazo kwa ushahidi zaidi.
Samaki aina ya DOLPHIN wakicheza na watoto.


Chui wakijiachia kitandani na mlezi wao.

Pamoja na kuwa na urafiki na Binaadamu hata wao kwa wao ni marafiki.