Tuesday, June 7, 2011

PICHA YA LEO

Ni kama huyu mtoto anasema " Aaah mzee...unanipa pipi? shuka uone home tulivyo majalala..hapa nilipo sina hata sare za shule, home hatujala tokea jana mchana".

WAJUE 10 WANAOWANIWA NA ARSENE WENGER.

Meneja wa timu ya Arsenal ya uingereza Arsene Wenger amnahusishwa na nia ya kuhitaji wachezaji ambao atawatumia kujenga kikosi cha timu ya Arsenal ambacho kimemaliza ligi na hali mbaya japokuwa kilikuwa kikiwania ubingwa kwa karibu zaidi, wachezaji ambao wapo kichwani mwa Wenger ni hawa wafuatao. 
1-Gervinho, mshambuliaji wa Lille ya ufaransa raia wa Ivory Coast mwenye umri wa miaka 24 ambaye anauzwa kwa dau la paundi za uingereza milioni 12-15.


2-Borjan Kric,Mshambuliaji wa Barcelona na raia wa uhispania mwenye umri wa miaka 20 dau lake ni paundi za uingereza milioni 16-18. 

3-Mamadou Sakho,mlinzi wa kati wa PSG na raia wa ufaransa mwenye umri wa miaka 21 dau lake ni paundi za uingereza milioni 12-18.

4-Jan Vertonghen,Mlinzi wa kati wa Ajax na raia wa ubelgiji, umri miaka 24,dau lake ni paundi za uingereza milioni 12-15.
5-Gary Cahill, Mlinzi wa kati wa Bolton na raia wa uingereza, umri miaka 25,dau lake ni paundi za uingereza milioni 15-20.

6-Phil Jones, Mlinzi wa kati wa Blackburn na raia wa uingereza, umri miaka 19, dau lake ni paundi za uingereza milioni 15-18.

7-Karim Benzema, Mshambuliaji wa Real Madrid na raia wa Ufaransa,umri miaka 23, dau lake ni paundi za uingereza milioni 20-26.

8-Christopher Samba, Mlinzi wa kati wa Blackburn na raia wa Congo, umri miaka 27, dau lake ni paundi za uingereza Milioni 8-12.

9-Radamel Falcao,Mshambuliaji wa Porto na raia wa Colombia, umri miaka 25, dau lake ni paundi za uingereza milioni 26.


10-Ricardo Alvarez, mshambuliaji wa pembeni wa Velez Sasfield na raia wa Argentina, umri miaka 23, dau lake paundi za uingereza milioni 6-12.

ARSENE WENGER
wakati huo huo wenger anatafuta mrithi wa Niclas Bendtner mbali na hao kumi katika kumrithi Bendtner wengine ni Jeremy Menez wa Roma ya italy, Hugo Rodallega waWigan Athletic,Hulk wa Porto F.C, Gonzalo Higuian wa Real Madrid na Eden Hazard wa Lille.

BURRESS AMALIZA KIFUNGO CHA MIAKA MIWILI.

Hatimaye mchezaji mashuhuri wa NEW YORK GIANTS siku ya jumatatu tarehe 6 mida ya saa tatu asubuhi aliachiliwa huru kutoka gerezani ikiwa ni miezi mitatu kabla ya kifungo chake kukamilika kutokana na kuonesha tabia njema akiwa gerezani na kurudi nyumbani kwake Florida baada ya kutumikia kifungo cha miaka miwili jela kwa kosa la kukutwa na silaha, ambapo siku ya tukio novemba 2008 akiwa katika klabu ya usiku jijini  New York kwa bahati mbaya risasi aliyoiweka kiunoni ilifyatuka na kumpiga katika mguu na kusababisha kukamatwa kwake na silaha kinyume na sheria.

                        Plaxico Burress akitoka Gerezani.

Plaxico Burress akizungumza na waandishi wa habari baada ya kutoka gerezani.

Plaxico Burress akiwa amembeba mwanae Elijah Burress baada ya kutoka gerezani.

        Plaxico Burress uwanjani kabla ya kukamatwa kwake.


Akiwa amevalia mavazi meusi,sweater jeusi,t-shirt nyeupe na pale chini ametupia sneakers nyeusi akiwa peke yake kutoka gerezani na kuangaza huku na huko na kumuona meneja wake Drew Rosenhaus na kumrukia kwa furaha."Napenda kumshukuru mungu kwa kunipa moja ya mitihani maishani mwangu" alisema burress, "Napenda niwashukuru wote kwa maombi na maneno ya kunitia nguvu nikiwa gerezani" aliongeza Burress. Burress ambaye mwezi wa nane anatimiza miaka 34 alijitupia ndani ya Range Rover na kuungana na mkewe tayari kwenda nyumbani kufungua ukurasa mpya wa maisha baada ya kifungo.
Burress alitoka gerezani akiwa amevalia kofia ya Philadelphia Phillies na inasemekana kuna uwezekano mkubwa akarudi kuichezea tena na wakati huohuo kuna uwezekano wa timu ya New York Jets wakamchukua ili kuziba pengo la Braylon Edwards aliyestaafu.