Wednesday, June 1, 2011

PICHA YA LEO

Maisha ndivyo yalivyo wakati mtu anatafuta gari la kutembelea anakosa wengine wanakula bata kama unavyoona pichani gari likiwa na bwawa la kupumzikia.

PILIPILI KICHAA NJIA NYINGINE YA KUPUNGUZA UZITO.

Maisha ya kila siku ya binaadamu kwa asilimia kubwa yametawaliwa na suala la kupata msosi ili kuweka sawa miili tayari kwa kuweza kuendelea kuishi na kufanya kazi za kila siku katika maisha ya mwanadamu, kuna suala la kufahamu ni vyakula gani vya kula na kwa wakati gani japokuwa hili lipo tofauti kwa watu yaani inategemeana na mwili wa mtu ambapo kuna miili ya watu hukubaliana na vyakula vya aina fulani na kukataa vyakula vya aina fulani japokuwa kuna watu wengine hali hii ni tofauti kwa maana ya kwamba wao hakuna kinachodunda miilini mwao kila kitu pwani
Ulaji wa vyakula vya mbalimbali bila kuucontrol ulaji husababisha baadhi ya watu kuwa na uzito kupita kiasi hali ambayo huwaweka katika hatari ya kupata magonjwa mbalimbali leo napenda niwashauri wale ambao wana uzito ambao haulingani na miili yao kuwa pilipili kichaa inaweza kukusaidia kupunguza uzito. Kwa mujibu wa tafiti zilizofanywa na wanasayansi na zimeandikwa katika makala ya pscology & behaviour, wataalamu wa mambo wanasema nusu kijicho cha chai chenye pilipili kichaa katika mlo wako humeng'enya kalori 10 zaidi ya kiwango cha kawaida katika milo 25.